Showing posts with label Video. Show all posts
Showing posts with label Video. Show all posts
Rais Magufuli ataka kiongozi huyu afukuzwe kazi
By
Edmo Online
at
Thursday, May 10, 2018
Rais Dkt. John Magufuli ameagiza wataalamu wote wa idara za maji katika halmashauri zote nchini kusimamiwa moja kwa moja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji ili kuimarisha usimamizi wa shughuli zinazofanywa na idara hiyo na kuwawajibisha wahusika pale miradi isipotekelezwa
Tazama video hapa Chini:-
Tazama video hapa Chini:-
Sugu na Masonga "wametoroshwa" Gerezani - Mbowe
By
Edmo Online
at
Thursday, May 10, 2018
Kufuatia kuachiwa huru kwa Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi na Katibu wa Chadema Nyanda ya Juu Kusini, Emmanuel Masonga kutoka Gereza la Ruanda, Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, amesema bado hawajafahamu ni taratibu gani zimetumika kuwaachia huru wakati kifungo chao kilikuwa bado.
“Katika mazingira ya kawaida, siku yao ya kifungo walichokuwa wamepewa kilikuwa kinaishia Juni 5, mwaka huu, lakini ghafla wakapewa taarifa kwamba wataachiwa leo. Hatuna hakika sana ni taratibu gani zimetumika kufupisha kifungo chao kwa sababu jambo hilo halijawekwa wazi.
“Tangu wamewekwa gerezani ni takribani miezi mitatu, mawakili wetu walifanya jitihada za kuhakikisha rufaa yao katika mazingira ya dharura inasikilizwa, lakini haikuwahi kupata jaji wala kusikilizwa kwa sababu kila jaji aliyepangiwa kesi hiyo alionekana ana udhuru,”alisema Mbowe.
Aidha, amesema wao wanaamini kesi hiyo haikuwa ya haki kwa sababu watuhumiwa walinyimwa dhamana mwanzoni, na kutokana na mazingira ya kesi yenyewe hawakutakiwa kupewa kifungo.
Pia amedai kwamba wataendelea na rufaa yao ili kuweka rekodi sawa na kudhihirisha kwamba Sugu na Masonga hawakuwa na makosa.
Sugu na Masonga walitiwa hatiani na kuhukumiwa kifungo cha miezi mitano jela Februari 26 mwaka huu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya kwa kutoa lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli kwenye mkutano wa hadhara walioufanya Desemba 30 mwaka jana eneo la Shule ya Msingi Mwenge jijini Mbeya.
Wawili hao wameshatumikia adhabu hiyo kwa siku 73 ikiwa ni zaidi ya robo ya kifungo chao. Tazama Video hapo chini:-
Sugu Azungumza Baada ya Kuachiwa Kutoka Gerezani
By
Edmo Online
at
Thursday, May 10, 2018
Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ ambaye ameachiwa huru leo Mei 10, 2018 kutoka katika Gereza la Ruanda jijini Mbeya alikokuwa amefungwa na Katibu wa CHADEMA Kanda ya Nyasa, Emmanuel Masonga, amefunguka na kuweka wazi kilichojiri.
Amesema hakuwa anafahamu iwapo angeachiwa huru leo hadi polisi walipomfuata na kumwambia ajiandae. Amedai mapaka sasa hafahamu imekuwaje hadi akaachiwa kwani ilijulikana ataachiwa Juni 5, ambapo kifungo chake kingekamilika.
“Watu wote walitarajia ningetoka jela mwezi Juni, lakini ghafla jana niliambiwa nijiandae kwamba kesho asubuhi (leo) natakiwa niachiwe huru, nilipotoka nje nikakuta askari wengi, nikaelekezwa kuingia kwenye gari la RCO mimi na mwenzangu Masonga, tukasindikizwa na maofisa magereza watano hadi nyumbani na kutukabidhi kwa familia.
“Watu wanauliza, imekuwaje? Lakini mimi ninawaambia sijui, kwa sababu haikuwa kazi yangu kufanya hesabu za magereza, hiyo ni kazi ya magereza, kwa sababu mimi ninachoamini sikutakiwa kuwa magereza in the first place, utumishi uko palepale kwa level ileile, tulikuwa na exposure sasa hivi tumeongeza experience,” amesema Sugu.
Sugu na Masonga walitiwa hatiani na kuhukumiwa kifungo cha miezi mitano jela Februari 26 mwaka huu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya kwa kutoa lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli kwenye mkutano wa hadhara walioufanya Desemba 30 mwaka jana eneo la Shule ya Msingi Mwenge jijini Mbeya.
Wameshatumikia adhabu hiyo kwa siku 73 ikiwa ni zaidi ya robo ya kifungo chao.
Tazama zaidi kwa kubonyeza Play hapa Chini:-
Chama cha MDA chafanya Makubwa Makete
By
Edmo Online
at
Wednesday, May 09, 2018
Chama cha Maendeleo Makete (MDA) jana kimekabidhi serikalini bati 150, mifuko 100 ya saruji pamoja na misumari Ya bati kilo 10 kwa ajili ya ujenzi wa bweni jipya la wavulana shule ya sekondari Mang'oto wilayani Makete mkoani Njombe
Tukio hilo limefanyika shuleni hapo ambapo Makamu mwenyekiti wa chama hicho Philipo Mahenge amesema mbali na Chama cha Maendeleo Makete kuguswa na tukio hilo pia waliwashirikisha wadau mbalimbali ambao nao wamechangia michango yao
Amesema hayo ni miongoni mwa malengo ya MDA kuleta maendeleo kwa wilaya ya Makete kwa kushirikiana na serikali na wadau mbalimbali wa maendeleo, huku akiwapongeza wananchi wa kata ya Mang'oto na Makete kwa ujumla kwa hatua ambazo wamekwisha zichukua tangu tukio la moto lilipotokea shuleni hapo
Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa bati hizo Mkuu wa wilaya ya Makete Mh. Veronica Kessy ameshukuru kwa msaada huo na kuendelea kuikumbusha jamii kuwa Maendeleo yataletwa na watu
Mkuu huyo wa wilaya ameshukuru kwa umoja, mshikamano na ushirikiano mzuri uliopo ndani ya chama hicho ambao umewezesha upatikanaji wa vifaa hivyo kwani uamuzi huo wa wanamakete waishio nje ya Makete kupitia MDA umefanikisha jambo hilo
Awali akisoma taarifa ya hatua mbalimbali zilizofikiwa baada ya bweni hilo kuungua Machi 12 mwaka huu, Afisa mtendaji Kata ya Mang'oto Bw. Mengi Chalamila amesema, shilingi milioni sita laki saba sabini na tatu elfu, pamoja na michango mingine ya vifaa kutoka kwa wadau imewezesha ujenzi wa bweni jipya kuanza ambapo ujenzi huo kwa sasa umefikia hatua ya lenta
Nao wanafunzi wanaosoma shuleni hapo wamesema wanashukuru kwa misaada inayoendelea kutolewa baada ya bweni hilo kuungua kwa kuwa yote hayo ni kwa ajili ya wao kusoma katika mazingira mazuri
Baadhi ya wazazi waliozungumza na mwandishi wetu wamesema msaada huo utawasaidia kwa kiasi kikubwa katika ujenzi huo ambao una umuhimu mkubwa katika elimu
Diwani wa kata ya Mang'oto Mh Osmund Idawa amesema vifaa hivyo walivyokabidhiwa vitafanikisha kuharakisha ujenzi wa bweni hilo
Machi 12 mwaka huu bweni la wavualana katika shule ya sekondari Mang'oto liliteketea kwa moto ambapo ujenzi wa bweni jipya unaendelea na inatarajiwa litakamilika Juni Mwaka huu
Tazama video Hizi:-
Steve Nyerere amvua nguo aliyezaa na Masogange, adai alichangia kulia tu msibani
By
Edmo Online
at
Wednesday, May 09, 2018
Msanii wa filamu bongo ambaye pia ni mchekeshaji maarufu Steve Nyerere, amefunguka juu ya tuhuma za kutofikisha fedha za michango zilizobaki kwenye msiba wa Agness Masogange, na kusema kuwa pesa hizo haziwezi kupewa familia.
Steve Nyerere amesema kwamba pesa hizo ambazo zimetajwa kuwa milioni mbili zimekusudiwa kumsaidia mtoto wa marehemu Sania, atakapoanza kidato cha kwanza hapo mwakani,
Steve Nyerere ameendelea kwa kusema kwamba familia ya Agness inapaswa kushukuru kwa mchango wao walioutoa kumzika ndugu yao, na sio kuanza kuulizia masuala ya pesa, kwani pesa hizo si kwa ajili yao bali ni kwa ajili ya mtoto.
Mkandarasi aliyemchefua Rais Magufuli akamatwa
By
Edmo Online
at
Tuesday, May 08, 2018
ZIKIWA zimepita siku sita toka Rais Dkt John Magufuli kuagiza vyombo vya ulinzi na usalama mkoa wa Iringa kuwakamata aliyekuwa mkuu wa chuo cha elimu Mkwawa Prof Pak Mushi na mkandarasi aliyehusika katika ujenzi wa ukumbi wa bilioni 8.8 katika chuo cha Mkwawa Iringa ,tayari jeshi la polisi mkoa wa Iringa limemkamata mkandarasi wa ujenzi huo .
Wakizungumza na waandishi wa habari jana kamanda wa polisi wa mkoa wa Iringa Juma Bwire na kamanda wa taasisi ya kupambana na rushwa nchini (Takukuru ) Aidan Ndomba walisema kuwa mtuhumiwa huyo Godwin Mshana wa kampuni ya Engineering Service Ltd mkazi wa Gangilonga mjini hapa alikamatwa toka Mei 3 mwaka huu ikiwa ni siku moja toka Rais alipotoa agizo hilo .
" Kufuatia agizo la Rais Dkt Magufuli kuhusu ujenzi wa ukumbi wa mikutano chuo kikuu cha Mkwawa uliojengwa chini ya kiwango agizo alilolitoa wakati akiwahutubia wanajamii wa chuo hicho tulifanya msako mkali na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo akiwa nyumbani kwake Gangilonga "A" "
Tazama Video Hii>>>>>>
Makubwa: Diwani aeleza anavyotafutwa anunuliwe
By
Edmo Online
at
Thursday, April 19, 2018
Diwani wa kata ya Matamba wilayani Makete mkoani Njombe Ephel Ng'ondya (CHADEMA) amesema amekuwa akipokea vishawishi vya kuhama kutoka kwa watu aliodai ni viongozi wa cha mapinduzi (CCM)
Bila kuwataja majina kwa sasa, Diwani huyo amesema yeye ni dhahabu na ndiyo maana anasakamwa ili anunuliwe
Tazama Video hii>>>>>>
Tazama Video hii>>>>>>
Kauli ya Mtoto wa Lowassa baada ya kumsikia Mwanadada akidai katelekezwa na Lowassa
By
Edmo Online
at
Wednesday, April 11, 2018

Salaams. Nimesikia mwanamama mmioja akiongea kuwa yeye ni ndugu yetu kule Dar es Salaam. Kwa taarifa tu sisi watu wa Monduli kwetu watoto ni baraka na neema, nimeshangaa ametukosa ukoo mzima kujitambulisha. Namwambia Paul Makonda, nimetoka naye mbali sana, nasikitika sana anavyotumia nafasi yake vibaya kwa manufaa anayoyajua. Makonda nimekulea.
Fred Lowassa- Monduli
Video ya mwanadada akidai ni mtoto wa Lowasa
Kinyambe "aonekana" Mbarali Mbeya
By
Edmo Online
at
Sunday, April 08, 2018
Aonekana akichekesha watu
Amani ukiiacha mbali hufanikiwi - Magufuli
By
Edmo Online
at
Sunday, April 08, 2018
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amesema kuwa mtu akiiacha amani mbali hawezi kufanikiwa katika mambo yake
Magufuli amesema hayo leo April 8, 2018 alipopata nafasi ya kuzungumza na wananchi na waumini aliposhiriki Ibada ya Kumsimika Mhashamu Isaack Amani kuwa Askofu Mkuu Jimbo la Katoliki la Arusha katika Kanisa la Mtakatifu Theresia la Mtoto Yesu Jimbo Kuu Katoliki jijini Arusha.
"Napofungua maombolezo nakutana na neno 'AMANI' naomba ni nukuu tu sitaweza kusoma yote "ukijiweka mbali na amani nikasahau kufanikiwa" kwa hiyo amani ukiiacha mbali hufanikiwi katika tafsiri yangu siyo nzuri kama ile ya 'philosophy' wanazozijua hawa wazee. Lakini katika Zaburi ya 122 mstari wa saba inasema 'Amani na ikae ndani ya kuta zako na kufanikiwa ndani ya majumba yako". Nikaenda Zaburi mstari wa nane inasema "Katika amani nitajilaza na kupata usingizi mara kwa mara maana wewe bwana peke yako ndiye unijaliae kukaa salama, nilipoenda Zabari ya 34 mstari wa 14 inasema "Uache mabaya ukatende mema utafute amani, ukaifuatie"alisema Magufuli
Rais Magufuli aliendelee kuhubiri amani kwa kuendelea kusoma masomo mbalimbali na vifungu mbalimbali kwenye vitabu vya dini ambavyo vimezungumzia masuala ya amani
"Nilipoenda Zaburi ya 119 ambayo ni ndefu zaidi nikachukua mstari wa 168 inasema "Wana wa amani nyingi waipendayo sheria yako wala hawana la kuwakwaza, ukienda Zaburi ya 29 mstari wa 11 neno amani pia lipo linasema "Bwana atawapa watu wake nguvu bwana atawabariki watu wake kwa amani" alisema Rais Magufuli
Mbali na hilo Rais Magufuli aliwapongeza maaskofu hao akiwepo askofu aliyemaliza muda wake pamoja na askofu Amani ambaye amesimikwa leo na kudai wamekuwa mstari wa mbele kupigania amani na kuhubiri juu ya amani.
Tazama video hii:-
Polisi Mkikuta bangi kamateni kijiji Kizima - Rais Magufuli
By
Edmo Online
at
Saturday, April 07, 2018
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewapiga marufuku askari polisi kufyeka mashamba ya bhangi, kwani hiyo siyo kazi walioajiriwa kuifanya
Rais Magufuli ametoa marufuku hiyo leo alipokuwa akihutubia wananchi waliofika kwenye sherehe za uzinduzi wa nyumba za askari polisi mkoani Arusha, zilizofanyika uwanja wa Sheikh Amri Abeid, na kusema kwamba jambo hilo sio kazi yao.
Rais Magufuli ameendelea kwa kusema kwamba kazi ya kufyeka mashamba ya bhangi ni ya wenyewe wananchi wanaolima bhangi hizo, na iwapo hawatamkamata mhusika wa shamba, basi wasombe kijiji kizima kwenda kulifyeka.
“Ninyi hamkuajiriwa kwenda kufyeka mashamba ya bhangi, makamanda wako na maaskari wako, wasikate mashamba ya bangi, hawakuajiriwa kufyeka bhangi, tumieni njia za intelijensia wenu mtamshika tu, kama shamba lipo karibu na kijiji, shika kijiji kizima, wazee, wanawake, watoto, ndio wakafyeke hilo shamba la bhangi, ila IGP usiwatume maaskari wako kufyeka bhangi, mtaumwa nyoka mle, mna uniform nzuri msidhalilishe jeshi kwa kufyeka bhangi, mimi nisingefyeka bhangi, wa kufyeka wapo”, amesema rais Magufuli.
Rais Magufuli ameendelea kwa kusema kwamba kazi yao ni kuhakikisha nchi inakuwa salama, hivyo masuala kama hayo sio majukumu yao pia ni udhalilishaji kwa jeshi la polisi.
Mtazame kwenye video hii hapa chini:-
Shabiki wa Simba aliyetoa taulo kwenye goli la njombe mji afariki dunia
By
Edmo Online
at
Friday, April 06, 2018
Taarifa isiyo rasmi Shabiki wa timu ya Simba mkoani Njombe alietoa kitaulo cha mlinda mlango wa timu ya Njombe Mji amekutwa amekufa nyumbani kwake mgenderwa leo huku sababu ya kifo hicho bado hakijafahamika.
Baada ya vurugu za kitaulo pale uwanjani Sabasaba juzi alikamatwa na polisi na kuachiwa jana.
Goli kipa wa Simba amepost kuonyesha kafariki, Tazma video hapo chini:_
Subscribe to:
Posts (Atom)













