Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo, amesema kuwa shughuli ya usimamizi na uratibu wa upatikanaji wa Katiba Mpya ya kisasa utasimamiwa na chama hicho na si vinginevyo.
CCM kusimamia mchakato wa Katiba Mpya
Tyson Nduguru rafiki wa marehemu MC Joe aliyepotea, apatikana
Kijana Tyson Nduguru, Rafiki wa karibu wa Joel Misesemo (MC Joel) aliyejirusha ghorofa ya 7 Makumbusho Dar es salaam na kufariki dunia, ambaye aliripotiwa kutoweka ghafla siku tatu tangu kutokea kwa kifo cha Joel, amepatikana jana June 1 2023.
Mke wa Tyson, Grace Rashid ameithibitisha kwa kusema; “Ni kweli Tyson amepatikana mchana wa leo (jana), mimi nilitoka kama kawaida nilikua naendelea na mizunguko akanipigia simu yeye mwenyewe.
“Nimefika nyumbani nimeshaonana nae ni mzima wa afya, mpaka sasa sijaongea nae lolote Watu wapo wengi tupo na familia, nitawajulisha zaidi baadae."
Ripoti za kutoweka kwa Tyson ziliibua maswali mengi kutokana na ukaribu wa wawili hao pamoja na matukio mawili tofauti yaliyowatokea kwa kupishana siku chache yakiwa na mazingira ya kutatanisha.
Nyama ya Nguruwe yaruhusiwa kwa masharti Ludewa
Baada ya kutolewa katazo la kutumia mazao yatokanayo na mnyama aina ya Nguruwe wilayani Ludewa mkoani Njombe ambalo lilitolewa kwa zaidi ya miezi miwili na nusu iliyopita kwa kile kilichodaiwa ni kutokana na uwepo wa ugonjwa wa homa ya Nguruwe hatimaye mnyama huyo ameweza kupunguziwa masharti ya katazo hilo baada ya kupungua kwa matukio ya ugonjwa huo.
Mwenyekiti CHADEMA Mbeya afutwa Uanachama
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Jimbo la Mbeya vijijini kimetangaza kumfutia uanachama Joseph Mwasote ‘China wa China’ ambaye ni Mwenyekiti wa chama hicho Mkoa wa Mbeya akidaiwa kuwa chanzo cha migogoro ndani ya chama hicho.
Tume: Kifo cha mwanafunzi UDOM hakina uhusiano na ajali ya Naibu Waziri
Tume ya Haki za Binadamu (THBUB) imetoa matokeo ya uchunguzi wa kifo cha mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Nusura Abdallah, huku ikidai hakikuwa na uhusiano wowote na ajali ya Naibu Waziri Dk Festo Dugange iliyotokea Aprili 25 kuamkia 26 mwaka huu.
Mwanaume aomba mahakama ivunje ndoa yake kutokana na uzuri wa mkewe
Mwanaume mwenye umri wa miaka 40 kutoka nchini Zambia, Arnold Masuka, ameiomba mahakama kuvunja ndoa yake kutokana na urembo wa kipekee alionao mke wake.
Masuka aliwashangaza viongozi na mashahidi katika mahakama ya mji mkuu wa Lusaka wakati alipomwambia hakimu kwamba urembo wa mkewe, Hilda Mleya umemfanya kukosa usingizi mara kadhaa.
Mzaliwa huyo wa Lusaka ameongeza kuwa amekuwa akiishi kwa hofu kwa muda mrefu ya kumpoteza mke wake kwa mwanamume mwingine, na hata anahofia kumuacha mke wake nyumbani peke yake anapotaka kwenda kazini kwa kuogopa huenda akashawishiwa na wanaume wengine.
Mwanaume huyo amemtaja mke wake, Hilda anayetokea Gokwe nchini Zimbabwe, kuwa ndiye mwanamke mrembo zaidi aliyewahi kukutana naye.
Katika mazungumzo na wanahabari baada ya kesi hiyo, Karani wa mahakama hiyo, Chenjerai Chireya amekiri kwamba hajawahi kushuhudia tukio kama hilo mahakamani katika miaka yake yote ya utumishi.
Wajawazito 2000 washiriki mbio za Mamathon Korogwe
Na David John, Tanga
WANAWAKE wajawazito zaidi ya 2000 wilayani Korogwe mkoani Tanga wameshiriki katika mbio za Mamathon ambazo zimefanyika kwa mara ya kwanza wilayani humo zilizoandaliwa na Mkuu wa Wilaya hiyo Jokate Mwegelo.
Lengo la kufanyika kwa Mamathon ni kutoa hamasa kwa wanawake wajawazito kujifungua salama na hatimaye kupunguza vifo vya mama na mtoto kama ambavyo Serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan imekuwa mstari wa mbele kupunguza vifo vinavyotokana na uzazi.
Akizungumza mbele ya wanawake hao, wananchi pamoja na viongozi mbalimbali kutoka ndani na nje ya Wilaya ya Korogwe , Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake (UWT) kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi ( CCM) Mary Chatanda aliyekuwa mgeni rasmi amempongeza Jokate kwa ubunifu huo.
“Tunakupongeza Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Jokate Mwegelo kwa kazi kubwa ambayo anaifanya na kote alikopita amekuwa akifanya kazi nzuri hivyo wananchi wa Wilaya ya Korogwe wajue wamepata jembe na ndio maana Rais Dkt Samia Hassan Suluhu ameendeea kumteua katika nafasi hiyo ya Mkuu wa Wilaya ya Korogwe .
“Wananchi wa Korogwe mmepata jembe na muendelee kumpa ushirikiano na sisi viongozi tutaendelea kumuunga mkono na katika hili la ambalo ameliazisha aendelee nalo kwani linagusa maisha ya wamama wajawazito na watoto moja kwa moja kulinda afya zao, ” amesema Chatanda.
Pia amewataka wananchi wa Korogwe kumtumia Mkuu wa Wilaya hiyo kwani ana mambo mazuri yatakayowezesha kuwaletea maendeleo na wao kama viongozi wa Chama na Serikali watatoa ushirikiano wa kutosha kuhakikisha anatekeleza majukumu yake vizuri.
Akifafanua kuhusu mbio za Mamathon amesema ni jambo jipya katika Wilaya ya Korogwe na Jokate ameonesha ubunifu mkubwa, hivyo anamshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kumteua Mkuu huyo wa Wilaya kwani mambo yamekuwa moto.
amewapongeza wanawake wajawazito pamoja na wote walioshiriki na kumaliza mbio hizo kwani kufanya mazoezi kwa mjazito kuna faida nyingi.”Kupitia mbio hizi kuna mama mjamzito mmoja amepelekwa hospitali na tunamuombea ajifungue salama.”
Amewataka kuhakikisha baada ya mbio hizo wanaendelea kushiriki mazoezi ,kuzingatia lishe Bora kipindi chote cha ujauzito wao jambo litakalosaidia kujifungua salama na kuwezesha mpango wa Serikali wa kupunguza vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga.
Pamoja na mambo mengine Chatanda amesema mbali ya mbio hizo, amepokea vifaa tiba kwa ajili ya Hospitali ya Wilaya ya Korogwe na hiyo ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Rais Samia katika kuboresha huduma za afya ikiwemo ununuzi wa dawa na vifaa tiba.
“Kuna kila sababu ya kumpongeza Rais Dkt Samia Kwa kazi kubwa anayoifanya katika sekta ya afya na kwa kipindi cha miaka miwili kwa nchi nzima ameboresha miundombinu kwenye sekta ya afya katika ngazi zote za Zahanati ,vituo vya afya ,Hospitali za Wilaya , na kungineko na kupeleka vifaa tiba Kwa ajili ya kutolea huduma za afya.”
Ametumia nafasi hiyo kutoa rai kwa wahudumu katika vituo vya afya Zahanati ,na Hospitali zote kuzingatia maadili ya kazi zao, na kuepuka na vitendo vinavyokwenda kinyume na maadili ya kazi wanayoifanya huko akitolea mfano vitendo vilivyojitokeza wilayani Kaliua mkoani Tabora na anashukuru Mkuu wa Mkoa wa Tabora Baltida Burhan kwa kuchukua hatua.
Mapacha wanachuo wafariki wakiogelea Ziwa Victoria
Kenny na Lenny Makomonde (24), mapacha na wanafunzi wa Chuo cha Mipango Kampasi ya Mwanza wamefariki dunia kwa kuzama majini walipokuwa wakiogelea ndani ya Ziwa Victoria.
Tukio hilo lililoacha simanzi na vilio miongoni mwa wanafunzi wa chuo hicho, ndugu, jamaa na marafiki limetokea jioni ya Mei 28, 2023 wakati wawili hao walipokuwa wakiogelea kwenye ufukwe wa Mihama Wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza.
Miili ya mapacha hao wanaosemekana kuwa na ujuzi na uzoefu wa kuogelea tayari imepatikana na kuopolewa kutoka majini na Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wakishirikiana na wananchi.
Mkuu wa Jeshi la Zima Moto Wilaya ya Ilemela, Insekta Deusdedith Rutta amesema taarifa za mapacha hao waliokuwa wanasoma kozi ya Mipango na Maendeleo kuzama maji ziliifikia Jeshi hilo Saa 1:00 usiku jana Mei 28, 2023.
‘’Juhudi za uokoaji zilishindikana kutokana na kiwazo cha giza,’’ amesema Inspekta Rutta
Amesema askari wa Zimamoto na Uokoaji walirejea eneo la tukio leo alfajiri kuendelea na uokoaji na kufanikiwa kuopoa miili ya mapacha hao Saa 5:00 asubuhi.
Makamba: Msituhukumu, tupeni muda miradi ikamilike
Waziri wa Nishati, January Makamba amesema takribani nusu ya miradi ya kimkakati iliyoainishwa na serikali ipo kwenye sekta ya nishati.
Wazika maiti si yao, wafukua na kuzika upya
Ukistaajabu ya Musa, utayaona ya firauni. Hivyo ndivyo unavyoweza kusema baada ya ndugu wa familia ya marehemu Gudluck Munuo (53), mkazi wa Kijiji cha Mese, Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro, kuchukua maiti ya mtu mwingine iliyokuwa imehifadhiwa katika Hospitali ya Kibong'oto na kwenda kuzika.
Awekewa chumvi kwenye tenki la pikipiki yake, Kisa anakemea Wizi
Kijana aliyetambulika kwa jina la George Mahundi mkazi wa kijiji cha Kiyogo kata ya Masasi Wilayani Ludewa Mkoani Njombe, amedai kuwekewa chumvi kwenye tanki pamoja na Injini ya pikipiki yake kutokana na kuwa mstari wa mbele katika kukemea matukio ya wizi kijijini hapo.
Msimamo wa CCM kuhusu Elimu ya Tanzania
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Daniel Chongolo ameeleza wazi Msimamo wa Chama hicho katika Sekta ya Elimu, kwa kubainisha kuwa maono ya CCM ni kuona Tanzania kama Taifa linakuwa na mitaala ambayo itatoa Elimu ya Taaluma ya Kujiajiri kuliko Kutegemea Ajira kwa Sekta ya Umma ama Binafsi.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Daniel Chongolo, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa Ndugu Daud Yasin (kulia) na Mbunge wa Jimbo la Mufindi Kusini (CCM) Ndugu David Mwakiposa Kihenzile pamoja na Viongozi na wanachama wengine wakitembea kwa miguu kuelekea Nyololo kuhudhuria kikao cha shina namba 27, ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya siku 7 mkoani Iringa .
Katibu Mkuu ameongozana na Wajumbe wa Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Katibu wa NEC Oganaizesheni Ndugu Issa Haji Ussi Gavu na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndugu Sophia Mjema.
Polisi: Kifungu cha sheria ya uchawi kipo na watu hupewa hukumu
Watu wengi wamekuwa wakiamini kuwa serikali haiamini uchawi na hakuna sheria inayombana mtu katika masuala hayo, lakini ukweli ni kwamba kifungu cha sheria ya uchawi kipo na watu hupewa hukumu pale wanapobainika kuhusika na masuala hayo.
Kwa upande wa Lucas Mahundi ambaye ndiye aliyejeruhiwa na watoto wake hao amesema kujeruhiwa kwake hakuhusiani na tuhuma za uchawi lakini wananchi wenzake walipinga kauli hiyo na kumtaka kuwa muwazi huku wengine wakieleza namna ambavyo wachawi hutumia mamba kuondoa uhai wao.
Adaiwa Kumuua Babake, Aupika na Kuula Mwili Wake
Mwanaume kutoka kijiji cha Giankaja, kaunti ya Tharaka Nithi NCHINI Kenya alitiwa mbaroni baada ya kudaiwa kumuua baba yake na kupika sehemu za mwili wake.
Mwanamume huyo kwa sasa anazuiliwa katika kituo cha polisi kaunti ya Tharaka Nithi.
Polisi walithibitisha kutokea kwa tukio hilo la kusikitisha wakisema mwathiriwa ambaye ni mzee mwenye umri wa miaka 70, aliripotiwa kutoweka kwa siku tatu. Msako ulifanyika katika kijiji kizima na wakazi wa eneo hilo katika juhudi za kumtafuta mzee huyo.
Baada ya saa kadhaa za msakao, upekuzi wao uliwaelekeza kwenye mtaro wenye kina kirefu ambapo waliupata mwili wa marehemu ambao tayari ulikuwa umeshaanza kuoza. Marehemu alikuwa amekatwa kichwa na sehemu za mwili wake kukatwa na miguu yake ikiwa kando ya mwili wake.
Walikimbia haraka kwa chifu wa eneo hilo ili kumjulisha kuwa wamempata mtu aliyepotea. Hata hivyo, waliporejea kwenye mtaro, mwili huo haukuonekana.
Wakiwa wamechanganyikiwa na jinsi mambo yalivyobadilika, wenyeji hao katika udadisi wao pamoja na polisi na chifu walitafuta ndani zaidi ya mtaro. Walizunguka kwenye mtaro wa kina kirefu uliowaelekeza kwenye nyumba ambayo polisi wanasema huenda ilikuwa ya mshukiwa. Walipofika katika nyumba hiyo, walishangaa kupata chungu cha kupikia kimejaa nyama na mboga.
Katika eneo la tukio, kulikuwa na fuvu la kichwa cha binadamu na nguo zilizojaa damu pamoja na viatu vya marehemu. Polisi walimhoji mshukiwa huyo kuhusu aliko baba yake lakini alibaini kuwa pia alikuwa hafahamu kwa kuwa anaendelea kumtafuta.
Sehemu nyingine za mwili zilizopotea ambazo ziligunduliwa kwanza na wenyeji zilipatikana zikiwa zimetupwa kwenye gunia na kufunikwa kwa mawe ndani ya Mto Nithi.
Mmoja wa wakazi wa eneo hilo ambaye alidai kuwa mshukiwa huyo alianza kuchimba mtaro huo mwaka 2017, alieleza kuwa mshukiwa na mwathiriwa wake walizozana kuhusu hali ya mtaro huo kabla ya kupotea. "Wawili hao walizozana baada ya mwanamume huyo kumzuia babake kukata nyasi za Napier kuzunguka mtaro," Johnson Mutembei mkazi aliambia jarida moja la eneo hilo.
Kwa sasa mshukiwa yuko rumande akisubiri kufikishwa mahakamani kujibu mashtaka ya mauaji.
Chanzo: TUKO.co.ke
Kichwa chazikwa baada ya mwili kuliwa na mamba
Jeshi la Polisi Mkoa wa Lindi limetoa taarifa ya mwanamke mkazi wa kijiji cha Nachui Kata ya Nyengedi Halmashauri ya Mtama mkoani Lindi akidaiwa kufariki dunia baada ya kuliwa na mamba katika mto lukuredi.