Halmashauri ambayo inakabiliwa na tatizo la njaa na kuhitaji chakula imetakiwa kuandika barua kwa Waziri Mkuu kupitia Wizara ya Sera, Bunge na Uratibu ambao ndiyo wenye jukumu la kutoa kibali kwa wataalamu kujiridhisha kama kweli kuna uhitaji wa chakula.
Simbachawene: Halmashauri yenye njaa iandike barua
Baba wa Watoto 102 Asema Ameshindwa Kuwalisha "Nimeelemewa jamani"
Kwa miaka mingi, kuwa na watoto 102 ilikuwa kama mzaha kwa Musa Hasahya Kasera mwenye umri wa miaka 68 kutoka kijiji cha Bugisa, wilaya ya Butaleja, mashariki mwa Uganda.
Alianza kuwa kivutio cha watalii baada ya habari kuenea kwamba ana wake 12, wajukuu 578, na kwamba hakumbuki majina ya wengi wa watoto wake. Sasa mwanamume huyo amejikuta katika taabu kwani ameshindwa kuwalisha wanawe na kuwajukumikia kwa sababu ya uidadi yao.
Kasera alifichua kuwa kwa sasa hana kazi jambo ambalo limekuwa changamoto kubwa kwake, Daily Nation iliripoti.
Hiyo inaeleza kwa nini hivi majuzi aliwataka wake zake wote wapange uzazi ili kukomesha kujifungua watoto zaidi kuepukana na changamoto za maisha. “Sitarajii kupata watoto zaidi kwa sababu nimejifunza kutokana na kitendo changu cha kutowajibika cha kuzaa watoto wengi ambao nimeshindwa kuwalea,” alisema mwanakijiji huyo.
Aliongeza kuwa afya yake inadhoofika na anahofia kwamba ekari mbili za ardhi anazomiliki hazitoshi kwa familia yake kubwa. Kasera pia alifichua kuwa wake zake wawili waliondoka kwa sababu hawakuweza kuendelea kukaa katika ndoa bila mambo ya msingi kama vile chakula na mavazi.
"Mwanzoni ilikuwa mzaha... lakini sasa hii ina matatizo yake," alilalamika. Siku zile akiwa mchanga ambapo Kasera alikuwa na biashara iliyonawiri ya kuuza ng’ombe na duka la nyama, wazazi walimpa binti zao awaoe.
Familia ilipozidi kuwa kubwa mzee huyo alishindwa kukumbuka majina ya wanawe wote na hivyo basi anakumbuka tu lile la kifungua mimba na kitinda mimba wake.
Watoto 102 wa Kasera ni kati ya umri wa miaka 10 hadi 50, wakati mke mdogo ana umri wa takriban miaka 35, wengi wao hawajasoma.
Mbali na watoto hao, mzee huyo hulazimika kushauriana na mmoja wa wanawe aitwaye Shaban Magino, mwalimu wa shule ya msingi mwenye umri wa miaka 30, ili kumkumbusha majina ya wake zake.
Chanzo: TUKO.co.ke
Lissu ashambuliwa kisa kudai alipata afueni baada ya kifo cha Magufuli
Kiongozi wa Upinzani nchini Tanzania, Tundu Lissu amesema kuwa yeye pamoja na viongozi wengine wa upinzani walipumua baada ya aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kufariki dunia.
Ndege ya Precision Air Yatua Kwa dharura, Nyingine yapata hitilafu
Shirika la Ndege la Presicion Air limethibitisha kuwa ndege zake mbili zimeshindwa kufanya safari zake kama kawaida baada ya ndege moja kupata hitilafu na nyingine kulazimika kutua kwa dharura.
Kupitia taarifa ya shirika hilo limesema moja ya ndege zake ilipata hitilafu ya kiufundi hivyo kusababisha kuchelewa na kuahirishwa kwa safari na nyingine ililazimika kutua kwa dharura baada ya kugonga kiumbe aina ya ndege wakati ikiruka kutoka Dar Es Salaam kuelekea Dodoma.
Amwagiwa maji ya Moto na Mpenzi wake, Kisa Mchepuko
Jeshi la polisi mkoani Mwanza linamshikilia Rehema Prosper (41), anayedaiwa kumjeruhi mpenzi wake aitwaye Timoth Samweli kwa kumwagia maji ya moto mgongoni, akimtuhumu kutoka kimapenzi na wanawake wengine.
Kamanda wa Polisi mkoani Mwanza Wilbroad Mutafungwa, amesema tukio hilo limetokea Januari 25, 2023, katika mtaa wa Bujingwa Manispaa ya Ilemela, ambapo mwanaume huyo alienda nyumbani kwa mpenzi wake huyo Rehema ndipo tukio hilo lilipotokea.
"Sasa akapata hasira na wivu ndipo akamuua kufanya tukio hilo la kikatili kwa sasa mwanaume huyo anaendelea kupatiwa matibabu katika kituo cha afya Buzuruga na hali yake inaendelea vizuri," amesema Kamanda Mutafungwa.
Katika hatua nyingine Kamanda Mutafungwa amezundua zoezi la uwekaji stika kwenye magari, pikipiki na bajaji huku akiwataka madereva kuhakikisha wanalipia fedha halali ya stika hizo.
Sheikh Alhad aliyetumbuliwa atoa kauli
Baada ya Sheikh Alhad Mussa Salim kutenguliwa nafasi ya kuwa Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kiongopzi huyo wa dini ya Kiislam amesema ataendelea kuwa ndani ya Baraza katika nafasi nyingine.
Tundu Lissu afungukia kauli ya 'kuunga mkono ushoga'
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Tanzania Bara, Tundu Antipasi Lissu amesema hajawahi kutaja popote kuwa anaunga mkono mapenzi ya jinsia moja (ushoga) ila ni kampeni chafu zilizoundwa na baadhi ya mahasimu wake ili kumchafua.
Polisi wamnusuru Mtuhumiwa wa Uchawi asipigwe mbele ya DC
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Tarime-Rorya limelazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya wananchi waliokuwa wakitaka kumshushia kipigo, Ajuza ambaye jina lake halijafahamika anayekadiriwa kuwa na umri wa zaidi ya miaka 60, wakimtuhumu kuhusika na kupotea kwa watoto watatu kwa njia za kishirikina.
Ajifungua mapacha watano, Wote wafariki Dunia
Furaha imegeuka kilio kwa familia ya Nakuru iliyobarikiwa na watoto watano katika hospitali ya kaunti ya Nakuru baada ya kifo kubisha hodi.
Watoto hao watanano, wasichana wanne na mvulana mmoja, wameripotiwa kufariki dunia ikiwa ni masaa chache tu baada ya kuzaliwa.
Daktari mkuu katika hospitali hiyo Aisha Maina amesema watoto hao walifariki dunia Alhamisi Februari 2, 2023
Mbunge wa Bahati Irene Njoki ni miongoni mwa wale ambao wamefikisha rambirambi kwa familia hiyo.
"Mambo yameisha vibaya, malaika hao watano walale pema," aliandika Njoki kupitia ukurasa wake wa mtandao. Wakenya walikuwa wamepokea taarifa za baraka hizo zilizobisha kwa Simon Ndung'u na mkewe Margaret Wangui.
Wangui alifika kwenye hospitali hiyo ya PGH na kujifungua watoto hao watano jambo ambalo liliipata familia yake kwa mshangao.
Alisema hakuwa ametarajia kupata watoto hao kwani ukaguzi wakati wa kliniki ulikuwa umeonyesha ana watoto watatau.
Chanzo: TUKO.co.ke
Aliyesababisha vifo vya walevi afikishwa kortini
Mahakama ya Hakimu Mkazi wilaya ya Lindi, imemsomea shtaka moja la mauaji mganga wa kienyeji aitwaye Shigela Ngelanija, anayetuhumiwa kwa kosa la mauaji ya watu watano ambao walimfuata awape dawa ya kunywa ili waache pombe, na baadaye kufariki dunia baada ya kunywa dawa hiyo.
Mwalimu afariki dunia akishangilia Matokeo
Mwalimu wa shule ya Sekondari ya Musoma Ufundi iliyopo Manispaa ya Musoma mkoani Mara Gaudence Aloyce (33), amefariki dunia kwa kugongwa na gari muda mfupi baada ya kumaliza sherehe ya kupongezana na walimu wenzake kufuatia shule yao kufanya vizuri kwenye matokeo ya kidato cha nne 2022.
Kiwanda cha pombe kali feki chanaswa
Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, imekamata kiwanda bandia kilichokuwa kikitengeneza pombe kali katika Mtaa wa Budeka, Kata ya Sima kwenye Halmashauri ya Mji wa Bariadi.
Wahusika wa kiwanda hicho bubu, walikodi moja ya nyumba katika mtaa huo na kuanza kungeneza pombe hiyo ambayo inadaiwa kutokuwa salama kwa walaji.
Taarifa zinaeleza kuwa bidhaa hiyo ilikuwa ikizalishwa kienyeji licha ya kuwa na nembo halali na stika za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), lakini pia bidhaa hiyo haina tarehe ya kuanza kutumika wala tarehe ya mwisho wa matumizi.
Mbali na hilo pombe hiyo inadaiwa ilikuwa ikitengenezwa kwa kuchanganywa maji na spirit, ambapo wahusika walikuwa wakitafuta chupa tupu za pombe kali na maboksi yenye nembo kisha kufanya mchanganyiko na kuupeleka sokoni.
Akizungumzia tukio hilo, kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya, Katibu Tawala Wilaya ya Bariadi, Nichodemus Shirima amesema wamewakamata watu wawili waliokuwa katika kiwanda hicho bubu huku akibainisha kuwa pombe ambayo ilikuwa ikitengenezwa kwenye kiwanda hicho ni hatari kwa walaji.
Ashikiliwa kwa kumuuwa mkewe na kumzika kisimani
Jeshi la Polisi Mkoani Arusha, linamshikilia Godfather Mndeme (36), mkazi wa Kijiji cha Mikungani katika Wilaya ya Arumeru mkoani Arusha, kwa tuhuma za kumuua mkewe, Furaha Akashi (40) kisha kumfukia kisimani.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Justin Maseju amethibitisha kutokea na kubainisha kuwa wanawashikilia watu wawili wanaodaiwa kuhusika na tuhuma hizo za mauaji yaliyopangwa kabla na baada ya utekelezaji wake huku akisema, “Kweli tukio limetokea na tunawashikilia watu wawili akiwamo mume wa marehemu wanaodaiwa kuhusika na mauaji hayo,” amesema Kamanda Maseju.
Wiki tatu zilizopita, Mndeme anadaiwa kumuua mkewe na kumfukia katika kisima hicho kisha kupanda mti na kumuajiri mtu awe anaumwagilia maji na kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi, Mwenyekiti wa Kijiji cha Mikungani, Idd Salum alisema mauaji hayo yanadaiwa kutekelezwa Januari 7 na walipolibaini hilo walilazimika kuufukua mwili wa marehemu ambao ulizikwa tena Januari 29 baada ya kukamilishwa na utaratibu wa kiuchunguzi na hatua za kisheria.
“Majirani hao walisema walimuuliza Mndeme kwa nini anatoa vyombo ndani na wakataka kujua alipo mkewe na akawajibu kuwa amesafiri kwenda Arusha hivyo anamfuata ila wakamzuia,” alisema mwenyekiti huyo na alisema majirani hao walienda kutoa taarifa ofisi ya kijiji hivyo akalazimika kufuatilia huku akimhoji Mndeme asema ukweli ili waweze kumsaidia kwani mke wake hakuonekana kwa muda mrefu kijiji hapo halafu ghafla anaonekana akihamisha vitu.
“Baadhi ya watu walitaka kumpiga huyo bwana ila alikiri kuwa amemuua mke wake baada ya kugombana na akaenda kutuonyesha alipomfukia ndipo tukatoa taarifa kituo cha polisi kwa hatua zaidi, Madaktari walibaini mwanamke huyo alipigwa na kuwekewa mti mgongoni kisha akafungwa na kumpiga kifuani, kichwani na kuvunjwa mguu,” alisema Salum.
Walipomaliza kufanya uchunguzi huo, alisema askari walitoa kibali cha mwili huo kuzikwa nao walimzika mahali alipokuwa amefukiwa na mumewe baada ya kumwita mchungaji aliyefanya sala na kumzika upya usiku.
Wanafunzi 1555 wa Msingi na 7457 wa Sekondari Wapata Mimba
Serikali imesema katika kipindi cha mwaka 2021 na 2022 Wanafunzi wa Shule za Msingi waliopata ujauzito ni 1,554 na Sekondari ni 7,457.
Atangaza kuuza Nguo za ndani za mume na mke baada ya kukataa kulipa kodi ya nyumba
Tangazo la madalali wa kupiga mnada mali zilizopigwa tanji katika kaunti ya Kisumu limezua vichekesho vikubwa kwenye mitandao ya kijamii baada ya kampuni moja ya madalali kwa jina Nyaluoyo kutangaza kupiga mnada vitu mbalimbali kwa nyumba ya mpangaji mmoja aliyekwama kulipa kodi ya nyumba hiyo.
Madalali hao wa Nyaluoyo waliweka tangazo la kupiga mnada mali hiyo kwenye gazeti la Jumatatu Januari 30, 2023. Baadhi ya mali ambayo madalali hao walitangaza kupiga mnada ni pamoja na chupi za mwanamume na mwanamke waliokuwa wamepangisha katika nyumba hiyo.
Nyaluooyo walitoa wito kwa umma kujitokeza ili kuweka maombi yao ili kuuziwa chupi hizo, zikiwemo 4 za mwanamume, 4 za mwanamke, mabegi mawili ya watoto, miongoni mwa vitu vingine.
Tangazo hilo lilikuwa linasema kuwa ni mzozo uliokuwa kati ya mmiliki wa nyumba na mpangaji wake kwa jina Zacharia Sichenje Masika.
Yeyote ambaye alitaka kuuziwa mali hiyo iliyopigwa tanji kutoka kwa mpangaji mkaidi alitaarifiwa kujitokeza katika ofisi za kampuni hiyo ya madalali mnamo Februari 7 saa tano asubuhi katika kaunti ya Kisumu.
Tangazo hilo lilionekana kwenye jarida moja la Jumatatu na wengi walilitupia vijembe kwa utani mwingi, wakisema kuwa hiyo ilikuwa kama njia moja ya kumdhalilisha mpangaji huyo na familia yake kwani hakuna mtu anayeweza kujitokeza kununua chupi zilizotumiwa wakati mpya sokoni huuzwa hadi kwa bei ya jioni ya shilingi mia tu.
Inasemekana kuwa mpangaji huyo alikuwa amekodisha chumba kimoja jijini Kisumu ambapo alikuwa anakitumia kama duka la kuuza nguo na malimbikizi ya kodi ya kila mwezi yalikuwa yamefikia laki moja na elfu ishirini ambayo alishindwa kulipa na mali yake yakapigwa tanjia alipofungiwa nje.
Chanzo;Radiojambo