Serikali imesema katika kipindi cha mwaka 2021 na 2022 Wanafunzi wa Shule za Msingi waliopata ujauzito ni 1,554 na Sekondari ni 7,457.
Wanafunzi 1555 wa Msingi na 7457 wa Sekondari Wapata Mimba
Atangaza kuuza Nguo za ndani za mume na mke baada ya kukataa kulipa kodi ya nyumba
.jpg)
Tangazo la madalali wa kupiga mnada mali zilizopigwa tanji katika kaunti ya Kisumu limezua vichekesho vikubwa kwenye mitandao ya kijamii baada ya kampuni moja ya madalali kwa jina Nyaluoyo kutangaza kupiga mnada vitu mbalimbali kwa nyumba ya mpangaji mmoja aliyekwama kulipa kodi ya nyumba hiyo.
Madalali hao wa Nyaluoyo waliweka tangazo la kupiga mnada mali hiyo kwenye gazeti la Jumatatu Januari 30, 2023. Baadhi ya mali ambayo madalali hao walitangaza kupiga mnada ni pamoja na chupi za mwanamume na mwanamke waliokuwa wamepangisha katika nyumba hiyo.
Nyaluooyo walitoa wito kwa umma kujitokeza ili kuweka maombi yao ili kuuziwa chupi hizo, zikiwemo 4 za mwanamume, 4 za mwanamke, mabegi mawili ya watoto, miongoni mwa vitu vingine.
Tangazo hilo lilikuwa linasema kuwa ni mzozo uliokuwa kati ya mmiliki wa nyumba na mpangaji wake kwa jina Zacharia Sichenje Masika.
Yeyote ambaye alitaka kuuziwa mali hiyo iliyopigwa tanji kutoka kwa mpangaji mkaidi alitaarifiwa kujitokeza katika ofisi za kampuni hiyo ya madalali mnamo Februari 7 saa tano asubuhi katika kaunti ya Kisumu.
Tangazo hilo lilionekana kwenye jarida moja la Jumatatu na wengi walilitupia vijembe kwa utani mwingi, wakisema kuwa hiyo ilikuwa kama njia moja ya kumdhalilisha mpangaji huyo na familia yake kwani hakuna mtu anayeweza kujitokeza kununua chupi zilizotumiwa wakati mpya sokoni huuzwa hadi kwa bei ya jioni ya shilingi mia tu.
Inasemekana kuwa mpangaji huyo alikuwa amekodisha chumba kimoja jijini Kisumu ambapo alikuwa anakitumia kama duka la kuuza nguo na malimbikizi ya kodi ya kila mwezi yalikuwa yamefikia laki moja na elfu ishirini ambayo alishindwa kulipa na mali yake yakapigwa tanjia alipofungiwa nje.
Chanzo;Radiojambo
Afiwa na Mke Siku 11 baada ya Harusi Yao
Mwanaume kwa jina la Twitter Idris Almustapha Daja (@almustapherr) ameibua hisia na taarifa za kifo cha ghafla cha mkewe mpya.
Kulingana na Daja, marehemu mkewe aliaga dunia siku 11 baada ya kufunga pingu za maisha katika sherehe ya maridadi.. Mwanamume aliyevunjika moyo alishiriki picha za harusi yao, ambapo alipiga naye ili kunasa wakati maalum ambapo rasmi alikuwa akiitwa mume. Jinsi Idris Almustapha Daja alivyonukuu picha za hisia.
''Innalillahi Wa'inna'ilaihi Raju'un. Nilimpoteza siku 11 baada ya harusi yetu. Tarehe 6 Januari 2023- 17 Januari 2023,'' alinukuu chapisho hilo. Wanandoa hao walipiga picha za kitamaduni kwa hafla yao. Walionekana maridadi kweli kweli. Zaidi ya watu 4,000 wameomboleza na Daja, huku wengi wakishiriki jumbe za kumpa pole kutokana na kifo cha marehemu mpendwa wake.
Afia gesti akiwa na mwanamke wake
Mfanyabiashara mwenye umri wa miaka 25, alipatikana amefariki katika chumba cha hoteli alichokuwa amekodisha kumumunya urojo na mpenziwe.
Ali Musstafa anaripotiwa kuanguka na kukata roho katika Hoteli ya Avenue Lodge mjini Arua, Uganda kutokana na kushindwa kupumua alikokuwa akirusha roho na mpenzi wake. “Mwathiriwa alianguka na kufia chumbani. Mpenziwe alienda na kuwajulisha wasimamizi wa hoteli ambao mara moja walitoa taarifa kwa polisi wa Arua. Eneo la tukio lilikaguliwa na kuhifadhiwa vizuri," ilisoma ripoti ya polisi.
Polisi katika Wilaya ya Arua eneo la Nile Magharibi walisema hawakupata dalili zozote za sumu, dawa za kulevya au athari zingine za mwili kutoka eneo la tukio.
"Hakuna chembechembe za matumizi mabaya ya dawa za kulevya, sumu au athari zingine za mwili zilizopatikana katika eneo la tukio. Mwili huo ulipelekwa katika Hospitali ya Rufaa ya Arua na kuchunguzwa,” msemaji wa polisi, SCP Fred Enanga alisema Jumatatu, kama alivyonukuliwa na Daily Monitor. Enanga anaamini kuwa mfanyabiashara huyo kutoka OZU, wadi ya Kenya katika Wilaya ya Arua alifariki dunia mwendo wa saa tatu usiku. Mwili wa marehemu baadaye ulichukuliwa kutoka chumba cha hoteli na kupelekwa kufanyiwa uchunguzi wa maiti. "Kifo wakati wa kujamiana kinaweza kutokea kwa sababu kadhaa, ambazo ni pamoja na mkazo wa mwili kutokana na shughuli hiyo au kwa sababu ya hali isiyo ya kawaida ," aliongeza.
Katika tukio sawia na hilo, siku tatu zilizopita mzee wa miaka 71, alipatikana amefariki kwenye gesti baada ya kurushana na mpenziwe mwenye umri wa miaka 22. Kulingana na uchunguzi wa polisi, mrembo huyo mwenye umri wa miaka 22, alichukuliwa kutoka Githurai na mzee huyo kabla ya kuelekea kwenye gesti. Wakiwa katika hali ya kujamiana, mwanamume huyo alisemekana kuanza kulalamika kuhusu matatizo kadhaa ya kiafya. Alikimbizwa katika Hospitali ya Aga Khan ambapo alithibitishwa kufariki baada ya kuwasili.
Chanzo: TUKO.co.ke
Aliyesombwa na mto Lindi akutwa kichwa na mifupa pekee

Mwili wa Mwanahawa Abdallah (65), mkulima na mkazi wa Kijiji na Kata ya Kiwalala, Halmashauri ya Mtama mkoani Lindi aliyepotea wiki iliyopita kwa kusombwa na maji kwenye Mto Lukuledi, umeonekana ukiwa umebaki kichwa na mifupa baada ya kuliwa na wanyama.
Mwili wa mtoto mchanga wakutwa shambani bila kichwa

Wakazi wa kijiji cha Gacuku katika kaunti ya Embu walipigwa na butwaa baada ya kukuta mwili wa mtoto mchanga ukiwa bila kichwa umetupwa shambani.
Watu watano wafariki kwa kunywa dawa ya kuacha pombe
Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama, Hassan Ngoma amesema Watu watano wamefariki dunia katika Kijiji cha Nambilanje Wilayani Ruangwa, Lindi baada ya kunywa dawa waliyopewa na Mganga wa tiba asili, Shigela Malehe(39), ili iwasaidie kuacha pombe.
DC mteule ambaye hakujitokeza kuapishwa ahojiwa kwa dakika 50
Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Japheth Maganga amesema kwa sasa hawezi kutoa sababu kwanini hajaripoti wilaya aliyopangiwa ya Kyerwa, Mkoa wa Kagera huku akihojiwa na Jeshi la Polisi, mkoani Tanga.
Mwenyekiti Chadema Mikumi atimkia CCM
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Mikumi, Bakari Hasani amekihama chama hicho na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kusema ameridhika na kazi zinazofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan na ameamua kumuunga mkono.
Amuua mkewe kwa jembe akimtuhumu kuchepuka
Polisi katika eneo la Navakholo, kaunti ya Kakamega wanachunguza kisa ambapo mwanamume mwenye umri wa miaka 67, anadaiwa kumuua mkewe mwenye umri wa miaka 54.
🔴Matokeo ya kidato cha nne 2022 kwa shule zote za Sekondari Wilayani Makete
Tazama hapa kuangalia matokeo ya kidato cha nne 2022 kwa shule zote za sekondari zilizopo wilaya ya Makete mkoani Njombe, kwa kubonyeza jina la shule husika.
🔴🔴Breaking News: Matokeo ya kidato cha nne 2022 yatangazwa, Angalia hapa kuyaona

‘Magari ya wagonjwa yasisafirishe maiti’

Wananchi wa Wilaya ya Mukono na Buikwe nchini Uganda wameiomba serikali kupiga marufuku magari ya wagonjwa kutumika kusafirishia maiti.
Mkazi wa Kijiji cha Lubumba wilayani Buikwe, Richard Tamale, alisema imekuwa mazoea kwa magari ya wagonjwa hasa yanayomilikiwa na wanasiasa kutumika kusafirishia maiti hali inayofanya jambo hilo kuwa kama sehemu ya kampeni zao za kisiasa.
“Fikiria kwamba imetokea dharura ya mgonjwa wakati dereva wa gari la wagonjwa ndiyo ametoka kushusha maiti, je, dereva atakuwa na muda hata wa kupulizia dawa ya kuua vijidudu gari yake? Kwa hiyo serikali lazima iingilie kati na kuzuia jambo hilo,” alisema.
Mkazi wa Kijiji cha Kisoga wilayani Mukono, Adams Lubinga, alisema si sahihi kuruhusu magari ya wagonjwa kusafirishia maiti kwa kuwa madereva hawataheshimu wala kujali wagonjwa wanaohitaji huduma ya dharura wakidhani ni sawa na kubeba maiti.
“Mara nyingi magari ya wagonjwa hayapewi nafasi na watumiaji wengine wa barabara kama madereva wa malori kwa sababu magari mengi ya wagonjwa yanatumika kwa shughuli nyingine ikiwemo kusafirisha maiti au kusafirisha watu wanaokwepa msongamano wa magari,” alisema Lubinga.
Mmoja wa madereva wa magari hayo ya wagonjwa, Fred Kiyimba, alikiri kuwa kubeba maiti kwenye magari ya wagonjwa ni kinyume cha sheria lakini mara nyingi madereva hujikuta njia panda katika hilo.
Kiyimba alisema baadhi ya magari hununuliwa na wanasiasa, hivyo wapiga kura wao wanadhani kuwa wana haki ya kuyatumia kwa jambo lolote.
Mbunge wa Manispaa ya Mukono, Betty Nambooze, ambaye anamiliki magari mawili ya kubebea wagonjwa, alisema ili kuepuka hali hiyo, alinunua gari maalumu la mazishi ili kusaidia wapiga kura wake.
Kutokana na hali hiyo, wananchi hao waliomba uongozi wa Manispaa ya Mukono kuiomba serikali kupitia Wizara ya Afya kutoa mafunzo ya huduma ya kwanza kwa madereva wa magari ya wagonjwa na namna ya kuhudumia masuala ya dharura.
763 wakamatwa kwa kutopeleka watoto shule

Zaidi ya wazazi 763 wamekamatwa katika operesheni maalum ya nyumba hadi nyumba, ya kuwasaka wazazi na walezi wasiopeleka watoto wao waliochaguliwa kuanza masomo ya kidato cha kwanza mwaka huu katika wilaya yaTunduru mkoani Ruvuma.
Ufafanuzi kwa nini Shaka anastahili kuwa mkuu wa Wilaya Bara

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kumteua aliyekuwa Katibu wa NEC wa Itikadi na Uenezi Komredi Shaka Hamdu Shaka katika nafasi ya Ukuu wa Wilaya ya Kilosa.
Wakosoaji wengi wamejikita katika Uzanzibari na Ubara na kushindwa kujadili uhalali wa Kikatiba na Kisheria juu ya nafasi ya Ukuu wa Wilaya na sifa za wateule.
Ibara ya 61 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeanzisha nafasi ya Mkuu wa Mkoa na Ibara ya 61 (3) imempa Rais Mamlaka kikatiba kuteua wakuu wa Mikoa ya Tanzania Bara kwa kushauriana na Waziri Mkuu na wake wa Zanzibar watateuliwa na Rais wa Zanzibar baada ya kushauriana na Rais wa JMT.
Ibara ya 61 inanukuu.-(1) Kutakuwa na Mkuu wa Mkoa kwa kila mkoa katika Jamhuri ya Muungano ambaye, bila ya kuathiri ibara ndogo ya (3), atakuwa ni kiongozi katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
(2) Wakuu wa Mikoa katika Tanzania Bara watateuliwa na Rais baada ya kushauriana na Waziri Mkuu.
(3) Wakuu wa Mikoa katika Tanzania Zanzibar watateuliwa na Rais wa Zanzibar baada ya kushauriana na Rais.
Ibara ya 145 ya Katiba imeanzisha Mamlaka ya Serikali za Mitaa ikiwemo ofisi za Wakuu wa Wilaya ambazo uteuzi na shughuli zake zimeainishwa na Sheria ya Tawala za Mikoa.
Sheria ya Tawala za Mikoa imeweka bayana kuwa Rais anaweza kugawa Madaraka yake katika ngazi za Mikoa kwa Wakuu wa Mikoa chini ya Kifungu cha 6 (1) cha Sheria ya Tawala za Mikoa na pia anaweza kukasimu madaraka yake katika ngazi ya Wilaya kwa Wakuu wa Wilaya chini ya Kifungu cha 13 (1) cha Sheria ya Tawala za Mikoa. Vifungu husika vimenukuliwa:-
6.-(1) The President may by writing under his hand and the public seal, delegate any of hiss functions and duties under any written law to any Regional Commissioner.
13.-(1) There is hereby established in respect of each district in Mainland Tanzania the office of District Commissioner.
(2) Subject to the Constitution, every District Com- missioner shall be a public officer and shall be ap- pointed by the President.
(3) Subject to this Act and to any other written law, the District Commissioner shall, in. the exercise of his functions under this Act be subject to the directions, guidance or
instructions of the Regional Commissioner of the region in which the district for which he is appointed is situated.
Kwa mantiki hiyo, Rais wa Jamhuri ya Muungano anaweza kukasimu madaraka yake ya Urais katika eneo la Mkoa au la Wilaya kwa mtu yeyote ambaye ni Raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila kujali ametoka upande upi wa Muungano.
Jambo ambalo watu wengi ama kwa kutokujua ama kwa lengo la kupotosha ni juu ya majukumu na nafasi zinazotambuliwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano.
Nafasi ya Ukuu wa Wilaya au Ukuu wa Mkoa ni Madaraka yatokanayo na Madaraka ya Rais wa Jamhuri hivyo kama Rais wa Jamhuri anaweza kutoka upande wowote wa Jamhuri, maana yake (impliedly) hata Mkuu wa Mkoa au wa Wilaya anaweza kutoka katika eneo lolote la Muungano vivyo hivyo kwa nafasi za Kazi katika masuala ya Muungano kama Fedha, Ulinzi, Mawasiliano n.k Mtanzania anaweza kufanya kazi upande wowote wa Muungano. Mifano ipo mingi ya Watanzania Bara ambao wameteuliwa katika nafasi nyeti na kubwa visiwani kuliko hata za uDC.
Vivyo hivyo nafasi za Ubunge wa Jamhuri, Mtanzania yeyote anaweza kugombea popote, hapa hakuna sababu ya kutumia nguvu kujadiliana ni suala la logic tu, Mtu unaishi Songwe huwezi tu kuamka asubuhi ukaenda kugombea Ubunge Kigoma, ndivyo ilivyo, kulalamika kuwa kuna wazanzibari wamepata nafasi za Ubunge bara ni ubaguzi usio na haya, swali la kujiuliza ni je kuna Mbara yeyote aliwahi kugombea ubunge Zanzibar akakataliwa, je, wanaolalamika wana ushahidi kuwa hakuna wabara ambao ni wabunge Zanzibar kwa kuchaguliwa kutokana na kukidhi sifa na vigezo?
Mamlaka ya uteuzi humteua mtu kwa vigezo vingi na sio kwa sababu ya eneo atokako, dini wala kabila yake, siku Rais wa Zanzibar akiona kuna Mbara mwenye sifa ya kuwa Mkuu wa Mkoa wa Wete ninaamini hatasita kufanya hivyo.
Kikatiba na Kisheria hakuna mahala popote ambapo Rais Samia amekiuka kumteua Shaka, malalamiko yaliyopo ni kelele tu za kibaguzi na kutokujua misingi ya kisheria.
Simba yatangaza CEO mpya
Uongozi wa Klabu ya Simba umefikia makubaliano ya kumuajiri Ndugu Imani Kajula kuwa Afisa mtendaji Mkuu (CEO) wa klabu hiyo kwa mkataba wa miezi sita.
Kajula anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Barbara Gonzalez ambaye alijiuzulu nafasi yake Desemba 2022
Kajula amewahi kuwa kwenye Kamati ya maandalizi ya Michuano ya Afrika kwa vijana chini ya miaka 17 akiwa na uzoefu kwenye masuala ya Uongozi wa mpira wa miguu
Aliwahi kuwa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Masoko na mawasiliano ya EAG Group akihudumu kwenye nafasi hiyo tangu mwaka 2013.
BIbi wa miaka 80 adaiwa Kujinyonga Hadi Kufa
Mahakama yamwachia huru anayedaiwa kumuua mhasibu
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam imemwachia huru, Omary Hassan maarufu kama Mbegu aliyekuwa anakabiliwa na shitaka la kumuua kwa kukusudia Mwasiti Yasin aliyekuwa mhasibu wa Kampuni ya Grants Care Limited, baada ya ushahidi wa upande wa mashitaka kushindwa kuthibitisha shitaka dhidi yake.
Akisoma hukumu hiyo jana, Hakimu Mkazi Mkuu, Renatus Rutta alisema wakati wa usikilizwaji wa shauri hilo upande wa mashitaka walipeleka mashahidi wanane.
Hakimu Rutta alisema katika ushahidi uliotolewa na mashahidi hao, hakuna sehemu ambapo mshitakiwa ameguswa moja kwa moja, hivyo alimwachia huru.
“Katika mashahidi ambao waliletwa na upande wa mashitaka kutoa ushahidi dhidi yake, hakuna ushahidi ambao umeweza kumgusa mshitakiwa, ninamwachia mshitakiwa huru,” alisema Hakimu Rutta.
Kwa mujibu wa hati inadaiwa kuwa katika eneo la Uhuru na Sikukuu, Omary Hassan maarufu kama Mbegu alimuua kwa kumshambulia kwa risasi Mwasiti Yasin.
Inadaiwa marehemu akiwa ni Mhasibu wa Kampuni ya Grants Care iliyoko eneo la Kariakoo, Dar es Salaam, akiwa njiani mtaa wa Uhuru /Swahili kuelekea katika benki ya Habibu Afrika akiwa na Sh milioni 7.2 alivamiwa na majambazi kisha walimpiga risasi nakuchukua fedha hizo.
Wanandoa watelekeza watoto wao watano
OFISI ya ustawi wa jamii katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga imeanza kuwatafuta wanandoa wanaodaiwa kutelekeza watoto wao watano.
Wazazi na watoto wao walikuwa wanaishi katika Kitongoji cha Mwabuluki Kijiji cha Ng’wang’osha Kata ya Nyamalogo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.
Ofisa Ustawi wa Jamii katika halmashauri hiyo, Kulian Mlalama alisema hayo jana alipoitembelea familia hiyo akiwa amefuatana na Ofisa Mthamini na Mfuatiliaji kutoka Shirika la Thubutu Africa Intiative (TAI) la wilayani Shinyanga, Paschalia Mbugani.
Mlalama alisema wazazi hao wanatafutwa hata kama wameachana ili wawapeleke shule watoto hao na watimize wajibu wa kulea kwa ujumla.
“Sisi tutawaandikisha shule, tumeanza kuwatafuta wazazi tulikwenda kwa ndugu zao kwenye kijiji jirani kupata mawasiliano lengo ni watoto wapate haki zao za msingi ikiwemo elimu,” alisema.
Mtendaji wa kijiji hicho, Nyosoku Wambura alisema walifanya uchunguzi na wakabaini kuwa mama wa watoto hao ameolewa na mwanaume mwingine mkoani Geita na baba yao hajulikani alipo.
Mbugani alisema kitendo cha kutelekeza watoto na kusababisha wakose haki ya kupata elimu ni ukatili.
Mlezi wa watoto hao, Joyce Robert alisema anaishi na mumewe, Mashimba Usumahu anayefanya vibarua vya kulima na kwamba wao wana watoto sita hivyo familia imewaelemea.
Kwa mujibu wa Joyce, Mwenyekiti wa kitongoji, Marco Luhende ndiye aliyewapeleka watoto waliotelekezwa waishi kwenye familia yake.
Wengi wafurika kumpokea Tindu Lissu
Hatimaye Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu amewasili leo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere akitokea Ubelgiji na kupokelewa na wafuasi wa chama hicho.
Mwanasiasa huyo nguli wa upinzani ambaye awali alikuwa Mbunge wa zamani wa Singida Mashariki na mwanasheria nguli, amerejea baada ya miaka mitano kuishi nje ya nchi.
Lissu aliwahi kuwa rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) amepokelewa na viongozi na wanachama wa Chadema.
Mamia ya wafuasi wa CHADEMA wamekusanyika nje ya lango hilo wakiimba na kucheza huku ngoma pamoja na mavuvuzela.
Hata hivyo Jeshi la Polisi limeimarisha ulinzi na kuhakikisha wafuasi hao hawaingii ndani ya eneo la uwanja na badala yake wanabaki nje ya lango kuu pembezoni mwa barabara ya Nyerere.
Pia hali ya ulinzi na usalama iliimarishwa ili kuhakikisha kuwa shamrashamra hizo zinamalizika bila ya kuwepo kwa fujo.
Kairuki awajia juu walimu wanaowalamba viboko kwa wanafunzi
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Angellah Kairuki,amewaonya walimu wanaokiuka Kanuni za Elimu za mwaka 2002 na kutoa adhabu kali kwa wanafunzi Serikali haitosita kuchukua hatua kali dhidi yao.
Waziri Kairuki ameyasema hayo Januari 25,2023 jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na Maafisa Elimu Kata, Wakuu wa Shule za Sekondari, Walimu Wakuu wa Shule za Msingi na Viongozi wa Elimu ngazi ya Halmashauri kwenye kikao kazi cha uboreshaji wa Usimamizi wa Elimu Msingi na Sekondari Jiji la Dar es Salaam.
Waziri ametoa rai kwa walimu kwa kukumbuka kuwa wamekasimiwa ya kuwa walinzi wa watoto wanapokuwa shuleni kwa hiyo wasiwe sehemu ya kuwafanya watoto kuwa watoro kupitia adhabu wanazozitoa zinazokiuka taratibu, miongozo na kanuni mbalimbali.
“Suala zima la adhabu ya Viboko shuleni linaongozwa na Waraka wa Elimu namba 24 wa mwaka 2002 na umeeleza bayana kabisa hivyo ni vyema walimu wakafuata taratibu zilizoanishwa kwenye Waraka namba 24 wa mwaka 2002 ambao umeeleza wazi ni nani mwenye Mamlaka ya kutoa adhabu ya viboko na viboko vingapi vinaruhusiwa na kwa utaratibu upi vinatolewa kwa wanafunzi.
“Hatusemi watoto wasichapwe lakini wachapwe kwa kufuata taratibu na vigezo na kwa mujibu wa miongozo iliyowekwa.” amesisitiza Waziri Kairuki.
Waziri Kairuki amesema kuwa mwongozo huo unaeleza wazi ni nani mwenye mamlaka ya kutoa adhabu ya viboko na viboko vingapi vinaruhusiwa na kwa utaratibu upi vinatolewa kwa wanafunzi.
Ameendelea kufafanua kuwa waraka huo na Kanuni za Elimu za mwaka 2002 lazima zifuatwe katika utolewaji wa adhabu ya viboko shuleni.
“Kwa Mujibu wa mwongozo huo umeelekeza adhabu hiyo ya viboko inaweza kutolewa pale ambapo umetokea utovu wa nidhamu uliokithiri au makosa ya jinai yaliyotendeka ndani au nje ya shule yenye muelekeo wa kuishushia heshima shule.
“Kwa mujibu wa waraka huo adhabu hiyo inavyotolewa lazima izingatie vigezo ikiwemo ukubwa wa kosa, umri, jinsi na afya ya mtoto na haipaswi kuzidi viboko vinne kwa wakati mmoja.
“Waraka huo umeeleza jinsi adhabu hiyo inapaswa kutolewa kwa mtoto wa jinsia ya kike na kiume. Kwa Mtoto jinsia ya kike adhabu inapaswa kutolewa mikononi, na kwa mtoto jinsia ya kiume ni kwenye makalio.
“Pia Waraka huo umeeleza kuwa mwenye mamlaka ya kutoa adhabu ya viboko ni Mwalimu Mkuu au Mkuu wa shule husika au Mwalimu mwingine atakayekuwa ameteuliwa tena kwa maandishi,” amesema.
Pia ametanabaisha kuwa kwa mtoto wa kike imeelekezwa aadhibiwe na mwalimu wa kike au labda tu kama shule hiyo haina mwalimu wa kike ndipo anaweza kuadhibiwa na mwalimu wa kiume.
Hata hivyo kumekuwa na video inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusiana na mwanafunzi kufanyiwa ukatili na mwalimu kwa kupewa adhabu isiyo na staa na kuibua hisia kwa wazazi.




.jpg)













