Ufafanuzi kwa nini Shaka anastahili kuwa mkuu wa Wilaya Bara


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kumteua aliyekuwa Katibu wa NEC wa Itikadi na Uenezi Komredi Shaka Hamdu Shaka katika nafasi ya Ukuu wa Wilaya ya Kilosa.


Wakosoaji wengi wamejikita katika Uzanzibari na Ubara na kushindwa kujadili uhalali wa Kikatiba na Kisheria juu ya nafasi ya Ukuu wa Wilaya na sifa za wateule.

Ibara ya 61 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeanzisha nafasi ya Mkuu wa Mkoa na Ibara ya 61 (3) imempa Rais Mamlaka kikatiba kuteua wakuu wa Mikoa ya Tanzania Bara kwa kushauriana na Waziri Mkuu na wake wa Zanzibar watateuliwa na Rais wa Zanzibar baada ya kushauriana na Rais wa JMT.

Ibara ya 61 inanukuu.-(1) Kutakuwa na Mkuu wa Mkoa kwa kila mkoa katika Jamhuri ya Muungano ambaye, bila ya kuathiri ibara ndogo ya (3), atakuwa ni kiongozi katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano.

(2) Wakuu wa Mikoa katika Tanzania Bara watateuliwa na Rais baada ya kushauriana na Waziri Mkuu.

(3) Wakuu wa Mikoa katika Tanzania Zanzibar watateuliwa na Rais wa Zanzibar baada ya kushauriana na Rais.

Ibara ya 145 ya Katiba imeanzisha Mamlaka ya Serikali za Mitaa ikiwemo ofisi za Wakuu wa Wilaya ambazo uteuzi na shughuli zake zimeainishwa na Sheria ya Tawala za Mikoa.

Sheria ya Tawala za Mikoa imeweka bayana kuwa Rais anaweza kugawa Madaraka yake katika ngazi za Mikoa kwa Wakuu wa Mikoa chini ya Kifungu cha 6 (1) cha Sheria ya Tawala za Mikoa na pia anaweza kukasimu madaraka yake katika ngazi ya Wilaya kwa Wakuu wa Wilaya chini ya Kifungu cha 13 (1) cha Sheria ya Tawala za Mikoa. Vifungu husika vimenukuliwa:-

6.-(1) The President may by writing under his hand and the public seal, delegate any of hiss functions and duties under any written law to any Regional Commissioner.

13.-(1) There is hereby established in respect of each district in Mainland Tanzania the office of District Commissioner.

(2) Subject to the Constitution, every District Com- missioner shall be a public officer and shall be ap- pointed by the President.

(3) Subject to this Act and to any other written law, the District Commissioner shall, in. the exercise of his functions under this Act be subject to the directions, guidance or

instructions of the Regional Commissioner of the region in which the district for which he is appointed is situated.

Kwa mantiki hiyo, Rais wa Jamhuri ya Muungano anaweza kukasimu madaraka yake ya Urais katika eneo la Mkoa au la Wilaya kwa mtu yeyote ambaye ni Raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila kujali ametoka upande upi wa Muungano.

Jambo ambalo watu wengi ama kwa kutokujua ama kwa lengo la kupotosha ni juu ya majukumu na nafasi zinazotambuliwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano.

Nafasi ya Ukuu wa Wilaya au Ukuu wa Mkoa ni Madaraka yatokanayo na Madaraka ya Rais wa Jamhuri hivyo kama Rais wa Jamhuri anaweza kutoka upande wowote wa Jamhuri, maana yake (impliedly) hata Mkuu wa Mkoa au wa Wilaya anaweza kutoka katika eneo lolote la Muungano vivyo hivyo kwa nafasi za Kazi katika masuala ya Muungano kama Fedha, Ulinzi, Mawasiliano n.k Mtanzania anaweza kufanya kazi upande wowote wa Muungano. Mifano ipo mingi ya Watanzania Bara ambao wameteuliwa katika nafasi nyeti na kubwa visiwani kuliko hata za uDC.

Vivyo hivyo nafasi za Ubunge wa Jamhuri, Mtanzania yeyote anaweza kugombea popote, hapa hakuna sababu ya kutumia nguvu kujadiliana ni suala la logic tu, Mtu unaishi Songwe huwezi tu kuamka asubuhi ukaenda kugombea Ubunge Kigoma, ndivyo ilivyo, kulalamika kuwa kuna wazanzibari wamepata nafasi za Ubunge bara ni ubaguzi usio na haya, swali la kujiuliza ni je kuna Mbara yeyote aliwahi kugombea ubunge Zanzibar akakataliwa, je, wanaolalamika wana ushahidi kuwa hakuna wabara ambao ni wabunge Zanzibar kwa kuchaguliwa kutokana na kukidhi sifa na vigezo?

Mamlaka ya uteuzi humteua mtu kwa vigezo vingi na sio kwa sababu ya eneo atokako, dini wala kabila yake, siku Rais wa Zanzibar akiona kuna Mbara mwenye sifa ya kuwa Mkuu wa Mkoa wa Wete ninaamini hatasita kufanya hivyo.

Kikatiba na Kisheria hakuna mahala popote ambapo Rais Samia amekiuka kumteua Shaka, malalamiko yaliyopo ni kelele tu za kibaguzi na kutokujua misingi ya kisheria.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo