BIbi wa miaka 80 adaiwa Kujinyonga Hadi Kufa


Mkazi mmoja wa kitongoji ya Bulengahasi, Kata ya Katoro, Wilaya ya Geita, Mkoani Geita anayefahamika kwa jina la Kwilavia Luvinza anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 80 amekutwa amejinyonga kwenye mti wa mwembe chanzo kikiwa bado hakijafahamika.


Mtoto wa mama huyo Mashaka Machibiya ameeleza tukio hilo lilivyotokea.

Nae Balozi wa shina namba 18 kijijini hapo ameelezea juu ya tukio hilo huku akisema kwa taarifa aliyopokea kutoka kwa Daktari ni kwamba mama huyo huenda ameuawa.

Wakazi wa Bulengahasi nao wamesikitishwa na tukio hilo huku juhudi za kulitafuta Jeshi na Polisi na kutolea ufafanuzi zikiendelea.

Chanzo: Storm FM


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo