Mkazi mmoja wa kitongoji ya Bulengahasi, Kata ya Katoro, Wilaya ya Geita, Mkoani Geita anayefahamika kwa jina la Kwilavia Luvinza anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 80 amekutwa amejinyonga kwenye mti wa mwembe chanzo kikiwa bado hakijafahamika.
Mtoto wa mama huyo Mashaka Machibiya ameeleza tukio hilo lilivyotokea.
Nae Balozi wa shina namba 18 kijijini hapo ameelezea juu ya tukio hilo huku akisema kwa taarifa aliyopokea kutoka kwa Daktari ni kwamba mama huyo huenda ameuawa.
Wakazi wa Bulengahasi nao wamesikitishwa na tukio hilo huku juhudi za kulitafuta Jeshi na Polisi na kutolea ufafanuzi zikiendelea.
Chanzo: Storm FM