Mwili wa mtoto mchanga wakutwa shambani bila kichwa


Wakazi wa kijiji cha Gacuku katika kaunti ya Embu walipigwa na butwaa baada ya kukuta mwili wa mtoto mchanga ukiwa bila kichwa umetupwa shambani.


Mwili huo ulipatwa na mwanamke mmoja ambaye alikuwa shambani mwake akivuna maharagwe alipoukanyaga ghalfa na kuita watu

Wanakijiji hao walisema kwa mshangao kuwa hawajawahi shuhudia tukio la kustaajabisha kama hilo, huku wakisema mwili huo ulikuwa na dalili za kukatwa na mtu wala si kuliwa na wanyama kama ambavyo ingesemekana.

Mkuu wa polisi katika Kaunti Ndogo ya Embu Mashariki Bw Emmanuel Okanda alisema uchunguzi umeanzishwa kuhusu kisa hicho.

“Tumeanza uchunguzi wa tukio hilo na tunatoa wito kwa wanakijiji kutusaidia kumfichua muuaji,” alinukuliwa na jarida moja la humu nchini.

Bw Okanda alisema maafisa wa upelelezi walikuwa wakishughulikia suala hilo kwa uzito unaostahili na hakuna jiwe litakaloachwa bila kugeuzwa.

"Hili ni suala zito na hatutapumzika hadi mhalifu atambuliwe na kufikishwa mahakamani," alisema Bw Okanda.

Tukio hilo linajiri wiki mbili tu baada ya tukio sawia kuripotiwa katika eneo la Loitoktok kaunti ya Kajiado ambapo mwili wa mtoto wa gredi 6 ulipatikana umefungwa ndani ya gunia.

Mtoto huyo alisemekana kung’olewa macho, kuvunjwa mguu mmoja na sehemu zake za siri zilikuwa zimeharibiwa vibaya sana dalili kuwa wauaji huenda walimbaka kabla ya kumuua na kufunga mwili wake ndani ya gunia kabla ya kuutupa shambani.

Alisema mwili huo umepelekwa katika hifadhi ya maiti ya Hospitali ya Rufaa ya Embu huku msako wa kichwa hicho ukiendelea.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo