Simba yatangaza CEO mpya

Uongozi wa Klabu ya Simba umefikia makubaliano ya kumuajiri Ndugu Imani Kajula kuwa Afisa mtendaji Mkuu (CEO) wa klabu hiyo kwa mkataba wa miezi sita.


Kajula anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Barbara Gonzalez ambaye alijiuzulu nafasi yake Desemba 2022


Kajula amewahi kuwa kwenye Kamati ya maandalizi ya Michuano ya Afrika kwa vijana chini ya miaka 17 akiwa na uzoefu kwenye masuala ya Uongozi wa mpira wa miguu


Aliwahi kuwa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Masoko na mawasiliano ya EAG Group akihudumu kwenye nafasi hiyo tangu mwaka 2013.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo