Uongozi wa Klabu ya Simba umefikia makubaliano ya kumuajiri Ndugu Imani Kajula kuwa Afisa mtendaji Mkuu (CEO) wa klabu hiyo kwa mkataba wa miezi sita.
Kajula anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Barbara Gonzalez ambaye alijiuzulu nafasi yake Desemba 2022
Kajula amewahi kuwa kwenye Kamati ya maandalizi ya Michuano ya Afrika kwa vijana chini ya miaka 17 akiwa na uzoefu kwenye masuala ya Uongozi wa mpira wa miguu
Aliwahi kuwa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Masoko na mawasiliano ya EAG Group akihudumu kwenye nafasi hiyo tangu mwaka 2013.