Chadema kuanza kufanya mikutano ya Hadhara

Msimamo huo umetangazwa Wilayani Sengerema na Mjumbe wa Kamati Kuu, John Heche kwa maelezo kuwa suala hilo ni Haki yao Kikatiba


Heche amesema “Ndani ya mwezi mmoja ujao tutatangaza ratiba na kuanza Mikutano ya Hadhara, mwaka 2022 hautaisha bila CHADEMA kufanya mikutano ambayo ni Haki ya Kikatiba na Kisheria kwa Vyama vyote vya Siasa”

Tangazo la CHADEMA limekuja kukiwa na vikao kadhaa vya Wadau wa Siasa kutafuta namna bora ya kuendesha shughuli zao ikiwemo Mikutano ya Hadhara iliyozuiwa na aliyekuwa Rais wa Awamu ya 5, Hayati John Magufuli Mei, 2016.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo