Mgombea Ajiondoa kwenye uchaguzi akihofia Wajumbe Kumshughulikia

Mmoja kati ya wagombea wa nafasi ya uwenyekiti wa chama cha mapinduzi (CCM) Babati vijijini Ezekiel Dangalo ameamua kujitoa katika uchaguzi kwa madai ya kuwa na hofu ya kushindwa baada ya kushindwa katika uchaguzi wa awali.


“Nimeamua kujiondoa baada ya kuona vichwa ni vilevile vilivyonipiga vibaya kwenye uchaguzi wa awali hivyo nimeogopa” amesema mgombea huyo.

Hata hivyo kwa mujibu wa katiba ya chama cha mapinduzi, mgombea haruhusiwi kujiondoa siku ya uchaguzi, hivyo wajumbe wanaweza wakaamua kumchagua ama wasimchague.

Leo oktoba 2,2022 chama cha mapinduzi kinachoongozwa na Mwenyekiti wake wa taifa Samia Suluhu Hassan, kinafanya uchaguzi kuchagua viongozi katika ngazi za wilaya ambao wataongoza kwa kipindi cha miaka mitano. 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo