Ispekta Generali wa Polisi
(IGP), Said Mwema.
Na Bryceson Mathias,
Mvomero
JESHI la Polisi wilayami
Mvomero, limefanikiwa kutuliza vurugu za uchaguzi wa kuwapata wajumbe wa
mabaraza ya katiba ya wilaya (Mamlaka za Serikali za Mitaa) na uendeshaji wake
uliotangazwa na tume ya mabadiliko ya katiba.
Uchaguzi huo uliokuwa
ufanyike jana Kichamgani Turiani, ulkwama kufanyika, baada ya kuibuka vurugu
wananchi wakimkataa Mwenyekiti wa Serikali ya kijiji hicho Bw. Damson Minja
asiwe Mwenyekiti wa kikao kwa sababu ameshindwa kusoma mapato na matumizi tangu
achaguliwe.
