Mchungaji aonya kauli ya Vyuma vimekaza

MCHUNGAJI wa Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Kijitonyama, Dar es Salaam, Eliona Kimaro, amesema kauli za ‘vyuma vimekaza’ na ‘pambana na hali yako’ ni za kuzimu na hazipaswi kuendelea kuwepo mwaka huu. 

Akihubiri wakati wa ibada ya mkesha wa Mwaka Mpya usiku wa kuamkia Januari 1 mwaka huu, Kimaro alisema kauli hizo zilitawala mwaka jana na si vema watu wakavuka nazo. “Mapepo ya mateso yanakuja mahali hadi yanatengeneza mapambio na watu wanasema usihangaike na mimi pambana na hali yako… ni sentensi za kuzimu. 

“Hizi sentensi hazitavuka 2018, nazifuta kwa damu ya Yesu,” alisema


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo