TANZIA: Mchoraji wa katuni za Sokomoko afariki dunia

Mchora katuni maarufu ya SOKOMOKO Thaddei Thomas Marealle, amefariki usiku wa kuamkia leo katika Hospital ya Kairuki, taratibu za mazishi zinafanyika nyumbani kwa kaka ake William G Marealle Mikocheni jijini Dar es Salaam


Marehemu alijipatia umaarufu kupitia Katuni za Sokomoko zilizokuwa zikichapishwa kupitia gazeti la Sani lililojipatia umaarufu sana miaka ya tisini na mwanzoni mwa miaka ya 2000

Kupitia gazeti hilo zilikuwepo katuni nyingine maarufu kama vile Kifimbo, Kipepe, Harakati a Pimbi, Ndumila kuwili, Lodi lofa, Madenge, Sukununu za babu Sani, Bush Star na Born Town.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo