Picha 20 za kilichotokea jana stendi mpya ya Mabasi Tandala Makete

 Basi la kampuni ya Mwafrika linalofanya safari zake Iringa-Makete likishusha abiria stendi mpya ya Tandala
 Wananchi waliohudhuria kikao cha maboresho ya stendi hiyo mpya
 Mkuu wa wilaya ya Makete mh Daud Yassin akizungumza kwenye kikao hicho

 Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Makete Bw. Francis Namaumbo akifafanua jambo kwenye kikao hicho
 Mkazi wa kijiji cha Tandala wilayani Makete Yusuf Kisimbilo akichangia hoja ambapo alisisitiza serikali kuboresha mifereji ya maji katika stendi hiyo
 Mama ntilie, Tabia Ilomo akizungumzia namna barabara ya kutokea kwenye stendi hiyo ilivyowekwa eneo la hatari

 Wananchi wakiendelea kutoa maoni yao





 Mtaalamu kutoka ofisi ya mhandisi wa ujenzi wilaya ya Makete Jumanne Majenzi akijibu hoja za wananchi katika kikao
 Basi likiingia kwenye stendi hiyo mpya
 Afisa biashara wa wilaya Edonia Mahenge akiendelea kujibu hoja zinazomuhusu katika kikao hicho

 Vibanda vya wafanya biashara vilivyopo kwenye stendi mpya ya Tandala

 Eneo la kutokea linalolalamikiwa kuwa na mteremko mkali
Mkuu wa wilaya ya Makete Daudi Yassin (kushoto) akiwa na diwani mteule wa kata ya Tandala Egnatio Mtawa

Kikao cha kupokea maoni ushauri na maswali kuhusu matumizi ya stendi mpya Tandala kimefanyika jana katika stendi hiyo

Kikao hicho kimewakutanisha wananchi na viongozi wa wilaya ya Makete ambapo pamoja na mambo mengine wamekubaliana kuboresha changamoto ndogondogo zilizojitokeza ili stendi hiyo ianze kutumika rasmi


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo