Dakika 24 za Tundu Lissu Nairobi leo, Ataja mambo ya Kutisha

Mnadhimu mkuu wa chama cha upinzani nchini kwa tiketi ya Chadema, Tundu Lissu amedai kuwa kuna dalili zinaonesha watu waliomshambulia kwa risasi mjini Dodoma mwaka jana walikuwa na uhusiano na serikali.
Lissu, amesema hayo alipozungumza na waandishi wa habari mjini Nairobi huku akionekana kuilaumu serikali kwa kuwakandamiza wapinzani.
Amesema anaamini shambulio dhidi yake lililenga kumnyamazisha kutokana na uokosoaji wake wa mara kwa mara wa serikali.

Mbunge huyo wa Singida Mashariki ametoa wito kwa Jumuia ya kimataifa kuingilia kati akisema kwa madai kuwa hali nchini Tanzania imebadilika.
Amesema,hadi sasa anaamini kuwa hakuna uchunguzi wowote unaofanywa kuhusu kushambuliwa kwake Septemba 7, mwaka jana.
Tazama video Hii hapa chini:-


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo