Breaking News : Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa ahamia CCM leo

Mwenyekiti wa baraza la Vijana Chadema (BAVICHA),Patrobas Katambi amehamia Chama Cha Mapinduzi (CCM).Katambi ametangaza kujiondoa Chadema leo Jumanne Novemba 21,2017 katika mkutano wa halmashauri kuu ya CCM unaoendeshwa na mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Dkt. John Pombe Magufuli jijini Dar es salaam.

Katambi alikuwa mgombea ubunge jimbo la Shinyanga Mjini katika uchaguzi mkuu mwaka 2015 akikabiliana na Stephen Masele (CCM) ambaye aliibuka mshindi huku Katambi akidai kuibiwa kura katika uchaguzi huo.

Mbali na Katambi makada wengine wa CHADEMA wameamua kurudi CCM.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo