Na Denis Mtima
KWA mara nyingine, mwigizaji wa filamu za nyumbani, Shamsa Ford ametangaza kufunga ndoa na mchumba’ke, Dickson Matoke aliyezaa naye mtoto na baadaye kuhitilafiana.
KWA mara nyingine, mwigizaji wa filamu za nyumbani, Shamsa Ford ametangaza kufunga ndoa na mchumba’ke, Dickson Matoke aliyezaa naye mtoto na baadaye kuhitilafiana.
Shamsa Ford.
Katika mahojiano, Shamsa alifunguka kuwa
ameamua kufanya hivyo kutokana na kukaa chini na kutafakari juu ya
maisha ya kukaa peke yake bila mwenzi wake huku baba wa mtoto wake
akionesha upendo wa dhati kwake na mwanaye.
“Nimeamua kufanya hivyo kutokana na namna baba wa mwanangu anavyoonesha upendo kwangu na hata kwa mtoto wetu (Terry), kwa kweli namshukuru Mungu nitakapomaliza Mwezi Mtukufu wa Ramadhani na muda si mrefu vikao vya harusi vinaanza,’’ alisema Shamsa.
Alipoulizwa kuwa endapo akiolewa ataacha uigizaji, Shamsa alifunguka: Mchumba’ngu ni mwelewa hana kizuizi katika kazi yangu ya sanaa. Cha msingi ni kutimiza wajibu wangu wa kifamilia.”
Shamsa amekuwa akitangaza mara kwa mara kuwa atafunga ndoa na Dick baada ya kuishi naye kwa muda mrefu lakini matangazo hayo huwa hayazai matunda