MWANAMUME mwenye umri wa makamo alifikishwa mbele ya mahakama ya Nakuru na kushtakiwa kwa kujamiiana na kondoo.
Barnabas
Njuguna, alishtakiwa kuwa mnamo Julai 23, 2013, katika shamba la
Nyaituga lililo Mirangine, Kaunti ya Nyandarua, alijamiiana na kondoo
aliyekuwa amefungwa katika shamba hilo linalomilikiwa na Joseph Mwangi.
Mahakama iliambiwa kuwa Bw Njuguna alipatikana akiwa amevua nguo za sehemu ya chini ya mwili akitenda kitendo hicho.
Alipokabiliwa,
alijaribu kutoroka na kumpelekea mlalamishi, Bw Mwangi, kukamata long’i
yake iliyokuwa chini ya magoti, hadi akamwangusha chini.
Mahakama
ilizidi kuambiwa kuwa Bw Mwangi alipiga kelele zilizopelekea majirani
kufululiza hadi bomani mwake na kumsaidia kumpeleka mshtakiwa hadi
katika kituo cha polisi.
Wanakijiji
walimwita daktari wa mifugo aliyemkagua kondoo huyo na kuthibitisha kuwa
mshtakiwa alijamiiana naye, kulingana na maelezo mbele ya mahakama.
Ghadhabu zilipozidi kupanda, wanakijiji waliamua kumuua Bw Njuguna, ingawa walizuiliwa walipokuwa karibu kufanya hivyo.
Polisi wa utawala waliowasili hapo kwa haraka walifanikiwa kumuokoa mshtakiwa huyo kutoka mikononi mwa wanakijiji.
Alipofikishwa
mbele ya Hakimu Mkuu Samuel Mungai, Bw Njuguna aliyeonekana akiwa
mwingi wa wasiwasi alikiri mashtaka hayo na kuachiliwa kwa dhamana ya
Sh200,000 au Sh100,000 taslimu, huku kesi hiyo ikipangiwa kusikizwa
Septemba 9.
NA KNA