ANUSURIKA KUUAWA BAADA YA KUFUMWA AKIFANYA MAPENZI NA KONDOO

 Nakuru
MWANAMUME mwenye umri wa makamo alifikishwa mbele ya mahakama ya Nakuru na kushtakiwa kwa kujamiiana na kondoo.
Barnabas Njuguna, alishtakiwa kuwa mnamo Julai 23, 2013, katika shamba la Nyaituga lililo Mirangine, Kaunti ya Nyandarua, alijamiiana na kondoo aliyekuwa amefungwa katika shamba hilo linalomilikiwa na Joseph Mwangi.

Mahakama iliambiwa kuwa Bw Njuguna alipatikana akiwa amevua nguo za sehemu ya chini ya mwili akitenda kitendo hicho.

Alipokabiliwa, alijaribu kutoroka na kumpelekea mlalamishi, Bw Mwangi, kukamata long’i yake iliyokuwa chini ya magoti, hadi akamwangusha chini.

Mahakama ilizidi kuambiwa kuwa Bw Mwangi alipiga kelele zilizopelekea majirani kufululiza hadi bomani mwake na kumsaidia kumpeleka mshtakiwa hadi katika kituo cha polisi.

Wanakijiji walimwita daktari wa mifugo aliyemkagua kondoo huyo na kuthibitisha kuwa mshtakiwa alijamiiana naye, kulingana na maelezo mbele ya mahakama.

Ghadhabu zilipozidi kupanda, wanakijiji waliamua kumuua Bw Njuguna, ingawa walizuiliwa walipokuwa karibu kufanya hivyo.
 
Polisi wa utawala waliowasili hapo kwa haraka walifanikiwa kumuokoa mshtakiwa huyo kutoka mikononi mwa wanakijiji.
 
Alipofikishwa mbele ya Hakimu Mkuu Samuel Mungai, Bw Njuguna aliyeonekana akiwa mwingi wa wasiwasi alikiri mashtaka hayo na kuachiliwa kwa dhamana ya Sh200,000 au Sh100,000 taslimu, huku kesi hiyo ikipangiwa kusikizwa Septemba 9.

NA KNA


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo