.jpg)
Kwa mara ya pili jina la Waziri mkuu wa zamani Edward Lowassa
limetajwa kwenye ripoti ya kitengo cha utafiti cha jarida la Economist
Intelligence Unit EIU kuwa ndiye mwanasiasa anayekubalika zaidi ndani ya
CCM kuwania Urais mwakani.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo ya EIU yenye makao yake makuu
London,Uningereza ilitolewa December 19 mwaka huu na ushindani
unaoendelea kwa sasa baina ya wanasiasa sita wanaodaiwa kuendesha
kampeni za kuwania urais mwakani utakigawa Chama hicho,lakini
hautakinyima ushindi.
Makada wa CCM wanaodaiwa kuwania kiti cha Jakaya Kikwete ni pamoja na
Lowassa,Waziri mkuu Pinda,Fredrick Sumaye,Willium Ngeleja,Bernad
Membe,Steven Wassira na January Makamba.
Ukimuacha Pinda makada waliosalia katika orodha hii wamekwishatiwa
hatiani na kamati kuu ya CCM kwa kuendesha kampeni za kuwanaia nafasi
hiyo kinyume na sheria jambo ambalo limezua mgawanyiko wa kimakundi na
kuhatarisha umoja ndani ya Chama hicho.
“CCM itagawanyika katika kumpata mshindi wa kiti cha urais,nakundi la
Waziri mkuu wa zamani Lowassa ndilo linaloonekana kuwa na nguvu kubwa
ya mgombea wake kuteuliwa kuwania Urais,,,hata hivyo Pinda anafanya
vizuri na sasa kundi lake ndilo linaloshika nafasi ya pili nyuma ya lile
la Lowassa”lilieleza jarida hilo.