Hospitali ya Wilaya ya Mbogwe Mkoani Geita ina tatizo kubwa na
ukosefu wa vyumba vya kuhifadhia maiti hali inayosababisha zihifadhiwe
kwenye korido.
Hali hiyo ilibainika baada ya mwalimu wa shule ya Msingi Kasandalala
Wilayani humo Laideth Constantine mwenye miaka 33 kuthibitika kuwa
alimnyonga mtoto wa miaka saba na maiti yake kuhifadhiwa kwenye korido.
Kutokana na tukio hilo Mganga mkuu wa Hospitali hiyo Cosmas Kilosa
alisema hospitali hiyo ina changamoto kubwa ya kukosa sehemu ya kutunza
maiti hali iliyosababisha maiti hiyo kuhifadhiwa kwenye korido.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita Joseph Konyo alisema mwalimu huyo
anashikiliwa na Polisi baada ya vipimo vya daktari kuthibitisha kuwa
mtoto huyo kanyongwa.
Alisema mwili wa marehemu ulikua umejaa damu nyeusi,uvimbe pamoja na
kutokwa na ulimi mrefu nje na inasemekana mwalimu huyo ndiye aliyehusika
na tukio hilo.
