BOB JUNIOR ATAJA SABABU ZA KUBADILISHA JINA LA STUDIO YAKE

Studio ya Bob Junior imebadilika kutoka ‘Sharobaro Records’ na kuwa ‘Sharobaro Music’.
 
Bob Junior ameiambia Kikwetu Blog kuwa sababu za kubadilisha jina hilo ni kutokana na kubadilika kwa muziki atakaokuwa akiutengeneza kama mtayarishaji wa muziki na pia kutokana na kununua vifaa vipya.
 
“Ilikuwa ni mahesabu ya kwangu mimi na kampuni yangu, tulikuwa tunataka kuibadilisha kuanzia muziki, sound kwasababu kuna vyombo vipya ambavyo vimekuja kutoka Marekani na pia nilikuwa nimetengeneza sound mpya siku nyingi,” amesema.
 
Mtayarishaji huyo wa muziki amedai kuwa uamuzi huo umekuja ili kuwathibitishia watu kuwa anaweza kufanya muziki wa aina mbalimbali.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo