Taarifa iliyotolewa na CHADEMA imesema kuwa jeshi la polisi limeagiza wabunge hao wakamatwe popote walipo na kufikishwa kituoni kutokana na kushindwa kufika katika wito huo leo.
Aidha viongozi wa CHADEMA akiwemo Mwenyekiti wa Chama hicho Mhe. Freeman Mbowe, Katibu Mkuu wa Chama hicho Dkt. Mashinji na Salum Mwalim ambao walifika polisi kuitika wito huo mapema leo waliachiwa majira ya mchana wakiwa hawajahojiwa kitu chochote na kuambiwa warudi tena Jumanne 27, 2018.
Mbali na hilo jeshi la polisi liliendelea kuwashikilia Mbunge John Mnyika na John Heche ambao walibaki kituoni hapo na kufanyiwa mahojiano na kisha baadae kuruhusiwa kuondoka
