MFANYABIASHARA AKUTWA AMEFARIKI KWENYE KITUO CHA MABASI YAENDAYO KWA KASI JIJINI DAR

Marehemu kama vile kalala kumbe ndiyo kafariki.Mmoja wa mashuhuda wa tukio.Mtendaji wa eneo hilo na baadhi ya Wasamaria wakiufunika mwili wa marehemu.Mtendaji wa kata ya Midizini-Manzese Bw. Penford Kizo akiwa mahali pa tukio.

KIJANA mmoja wa kiume aliyedaiwa kuwa ni mfanyabiashara ndogondogo amekutwa amefariki katika kituo cha mabasi yaendayo kasi Manzese, jijini Dar, leo asubuhi.  Inasemekana vijana wengi huwa wana tabia ya kulala ndani ya vituo hivyo kwa hiyo watu iliwachukua muda mrefu kubaini kama amefariki.

Kwa mujibu wa mtendaji wa serikali wa Kata ya Midizini-Manzese, Penford Kizo, wa eneo hilo na mashuhuda wengine, kifo cha kijana huyo hakijafahamika kimesababishwa na nini.
TAZAMA VIDEO HAPA CHINI:-
(Picha / Habari: Gabriel Ng’osha na Mussa Mateja / GPL)


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo