BAJETI YA MWAKA 2014/2015 HUENDA IKASHINDWA KUTEKELEZEKA, SERIKALI YATAHADHARISHWA

Kamati ya bunge la bajeti imetaadharisha serikali kuwa bajeti ya mwaka 2014/15 uenda ikashindwa kutekelezeka toka siku ya kwanza kutokana kuwepo kwa malimbikizo makubwa ya madeni ya zaidi ya trilioni 2.9 ambayo ni sawa na asilimia 4 ya pato la taifa.
 
Akiwasilisha taarifa ya kamati ya bunge bajeti kuhusu hali ya uchumi wa taifa na mpango wa maendeleo wa taifa kwa mwaka 2014/15, mwenyekiti wa kamati ya bajeti Mhe.  Andrew Chenge amesema tatizo la kutosimamiwa kwa umakini matumizi ya serikali kumesababisha kuongezeka kwa matumizi kila mwaka na malimbikizo ya madeni  kutoka bilioni 611.4 hadi trilioni 2.09 kutokana na kutolipwa katika bajeti ya kila mwaka. 

Msemaji mkuu wa kambi ya rasmi ya upinzani bungeni Mhe.  Esther Matiko akiwasilisha mpango wa maendeleo wa taifa mwaka 2014/15 amesema mpaka sasa serikali haijawa na uhalisia wa bajeti yenye lengo la kupunguza umasikini kwa Watanzania yenye mtazamo wa kuwawezesha watu masikini, wajasiliamali na walaji. 

Kwa upande wake msemaji mkuu wa kambi ya upinzani upande wa fedha Mhe.  James Mbatia amesema tarakimu zilizowasilishwa bungeni zimeonyesha kuwa serikali imeweka kipaumbele zaidi katika matumizi ya kawaida kuliko ya maendeleo na kutaka deni la taifa litenganishwe na matumizi mengine yanayohusu mfuko mkuu wa hazina hatua mbayo mpaka sasa serikali haijatoa taarifa fasaha ya utekelezaji wa mapendekezo hayo. 

Aidha wakichangia mjadala wa bajeti kuu baadhi ya wabunge wameitaka serikali kuwekeza katika utafiti wa kila tatizo na kutupia lawama baadhi ya viongozi kutokuwa wabunifu wa katika kuongeza mapato na badala yake kung’ang’ania vyanzo vilevile vya mapato ikiwemo Juisi na Soda.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo