WAHARIRI WAKUMBUSHWA HABARI ZA UCHUNGUZI ZIZINGATIE MAADILI

WAHARIRI wa vyombo mbalimbali vyombo vya habari nchini, wametakiwa kujilinda wakati wa kutekeleza majukumu yanayogusa maslahi ya umma, zikiwemo habari za uchunguzi ambazo mara kwa mara zimekuwa kikwazo katika kutekeleza majukumu yao na haki za binadamu. 

Aidha, wametahadharishwa kujilinda katika kipindi cha matukio maalumu yanayotokea nchini, ikiwemo suala la kupata Katiba Mpya na Uchaguzi Mkuu unaotegemewa kufanyika mwaka 2015 kutotumiwa na wanasiasa na makundi mbambali katika jamii kwa kuzingatia maadili ya kazi zao. 

Wakiongea katika mafunzo yaliyoratibiwa na Mtandao wa kutetea haki za Binadamu (Tanzania Human Rights Defenders Coalition-THRDs Coalition, jana Juni 15, 2014 baadhi ya wahariri wa vyombo hivyo wamesema pamoja na masuala ya usalama kuwa nyeti, matatizo yanayotokana na madhara ya kiusalama wakati wa kutekeleza majukumu yanayoihusu jamii, pia serikali inatakiwa kutambua umuhimu wa suala hilo ili kuondoa changamoto zinazojitokeza. 

"Maadili katika mazingira tete, katika kipindi cha uchaguzi yanatikwa kuzingatiwa ikiwemo dhima ya maadili ya mwandishi katika taaluma ili kuripoti masuala ya ngazi tofauti na kufanya utafiti kwa kuzingatia taaluma ikiwemo suala la haki za binadamu" walikaririwa

Wamesema kuwa, sula la utetezi wahaki za binadamu linatakiwa kupewa kipaumbele katika kuuhabarisha umma juu ya mambo yanayoendelea nchini, hususani katika kipindi cha chaguzi mbalimbali ikiwemo uchaguzi mkuu utakaofanyika mapema mwaka ujuao 

Hata hivyo, wamesema kumekuwepo na tatizo la kuwepo na usiri wakutoa taarifa ambazo wananchi wanatakiwa kuzijua, na pindi uchunguzi wataarifa hizo unapofanywa na waandishi habari hupata vitisho na kuacha taarifa hizo kuendelea kugubikwa na utata huku baadhi watu wakiendelea kujinufaisha kupitia mali za umma. 

Awali Mratibu wa Mtandao huo, Onesmo Olegurumwa, alisema kuwa, mafunzo hayo yamewawezesha wahariri wa vyombo hivyo kuwa na uwezo wa kujilinda na kutathimini athari mbalimbali kuhusu namna ya kujilinda wawapo kazini na kujiepusha na masuala ya rushwa kwa manufaa ya mwandishi mwenyewe na Taifa kwa ujumla.

Mafunzo.
Akifunga mafunzo hayo yaliyofanyika Juni 13-15, Katibu Mtendaji wa Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari Nchini (Moat), Henry Muhanika, amesema mashirika yasiyo ya kiserikali yanayoshughulikia masuala ya utetezi, kujilinda, na kujikinga na madhara yanayosababishwa na ukiukwaji wa haki za binadamu, mashirika hayo kwa kushirikiana na wadau wengine wanatakiwa kutetea haki za binadamu likiwemo la wananchi kupata haki ya kuhabarishwa kwa habari zinazowagusa moja kwa moja. 

"Unapo ripoti masuala yanayomgusa mtu kwamfano amekamatwa akijishughulisha na wizi wa meno ya Tembo ni dhahiri kuwa hamtaelewana lakini kwa mafunzo mliyopata ninajua tumepata mbinu nyingi sana za kujikinga mahali pa kazi" alisema Muhanika.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo