RAIS KIKWETE AMUAGIZA MKUU WA MKOA WA NJOMBE KUFUATILIA WALANGUZI WA PARETO MAKETE


Rais Jakaya Kikwete Amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Njombe Keptein Mstaafu Aseri Msangi Pamoja na Watendaji Wake Kufuatili Shilingi Bilioni Kumi Zilizotolewa na Serikali Kwa Ajili ya Kuwalipa Wakulima wa Mahindi Wilayani Ludewa Ambao Wanaidai Serikali.

Aidha Rais Kikwete Pia Imeitaka Halmashauri  ya Makete Kwa Kushirikiana na Uongozi wa Mkoa  wa Njombe Kuwabana  Watu Wanaonunua Zao la Pareto Kutoka Kwa Wakulima Bila Kufuata Taratibu Zinazohusika na Kukwepa Kulipa Kodi na Kuwakandamiza Wakulima wa Zao Hilo.

Akiongea Wakati wa Majumuisho ya Ziara Yake ya Kikazi  ya Takribani Siku Sita Mkoani Njombe Kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe Rais Kikwete Ameruhususu Sekta Binafsi Kununua Mahindi ya Wakulima Yaliyosalia Kwa Wakulima.

Halikadhali Rais Kikwete Amewataka Viongozi wa Mkoa wa Njombe Kuendelea Kusisitiza Mazao ya Biashara Ikiwemo Miti ya Mbao ,Kahawa ,Matunda na Mbogamboga Pamoja na Kufufua Zao la Pareto

Akielezea Kuhusu Miundombinu Mbalimbali Mkoani Njombe Rais Kikwete Amesema Serikali Iko Katika Mchakato wa Kuhakikisha Wananchi Wanapata Huduma za Umeme,  Maji, Mawasiliano, Afya Pamoja na Ujenzi wa Barabara za Lami Zinazounganisha Makao Makuu ya Mkoa wa Njombe na Wilaya Zake Kupitia mpango wa Matokeo Makubwa Sasa .

Rais Jakaya Kikwete Hii Leo Jumatano Amehitimisha Ziara Yake ya Kikazi ya Siku Sita Kwa Kufanya Majumuisho  ya Sehemu Zote Alizotembelea Katika Wilaya za Mkoa wa Njombe Huku Akiwapongeza Wananchi Kwa Kushirikiana na Serikali Katika Shughuli za Maendeleo

NA MICHAEL NGILANGWA


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo