SHAROMILIONEA, ambaye kwa sasa ni marehemu aliyefariki kwa ajali ya
gari akielekea kijijini kwao lusanga, alionyesha umahiri mkubwa wa
uigizaji muda mrefu kupitia filamu ya Safari ya Adili filamu iliyoigzwa
kwa umahiri mkubwa na kuwashirikisha wasanii wenye uwezo akiwemo
marehemu Sharomilinea, ambaye kwa kiwango fulani kama alitabiri kifo
chake.
Sharo akitumia jina la Mkieti alijikuta akimtamani Jini na kupanga kuoana na jini Siti baada ya mtoto wa mfalme, Sharo kukubaliwa kumuoa jini alipewa sharti la kufa ndipo amuoe Siti na kweli sharo alifariki katika filamu hiyo na kuishi na jini, kuna maneno alkiyaongea yanatia simanzi.
Sharo akitumia jina la Mkieti alijikuta akimtamani Jini na kupanga kuoana na jini Siti baada ya mtoto wa mfalme, Sharo kukubaliwa kumuoa jini alipewa sharti la kufa ndipo amuoe Siti na kweli sharo alifariki katika filamu hiyo na kuishi na jini, kuna maneno alkiyaongea yanatia simanzi.
Katika filamu ya Safari ya Adili Sharo kaigiza kama mganga wa
kienyeji ambaye alitimua mbio baada ya kuona waganga wenzake wakiuawa
baada ya kushindwa kumtibia mke wa Mfalme aliyekuwa mgonjwa sana Sharo
akiwa polini kajificha anakutana na kundi la mtoto wa mfalme Adil
anayesafiri safari ya mbali kutafuta dawa ya mama yake akiwa na walinzi
wa mfalme.
Mtayarishaji wa filamu ya Adil Gumbo K anasema kuwa filamu hiyo
ilichelewa kutoka kwa sababu alikuwepo nje kwa masomo hata alivyorudi
alisikitika kwa kifo cha Sharo kilichomsikitisha ndipo rafiki yake
Bendera alipomuomba aitoe filamu hiyo kwa jamii na kubaini filamu ya
kwanza kabisa ya Sharomilionea kuigiza akiwa bado mdogo sana.
Filamu ya Safari ya Adil inatarajia kutoka hivi karibuni na
kusambazwa nchi nzima Wapenzi wa filamu wajiandae kumuona Sharomilionea
katika filamu ya kiasili kazi iliyo bora, wengi wanamjua Sharo kupitia
komedi zilimpa jina kutoka na staili yake ya Oooh mamaa!