LOVE & POWER YA KANUMBA KUZINDULIWA APRIL 12.


Steven Kanumba
Marehemu Kanumba Mwigizaji wa filamu Swahiliwood.

FILAMU ya mwisho kuigizwa na msanii nguli wa filamu Swahiliwood marehemu Steven Kanumba ‘Kanumba the Great’ iliyopewa jina la Love and Power inatarajia kuzinduliwa kwa aina yake baada ya wasanii kutoka Afrika magharibi kuarikwa kwa ajili ya tukio hilo la kuingia sokoni filamu ya mwisho ambayo wengi wanaisubiri kwa hamu ili waone kazi hiyo.


.
steven Kanumba
Enzi zake marehemu Kanumba akiwa katika moja ya filamu zake.
Steven Kanumba
Marehemu Kanumba katika pozi.

Akiongea na FC mratibu wa tukio hilo Mosses Mwanyilu amesema kuwa msanii huyo alikuwa ni kipenzi cha wapenda filamu Bongo na nje ya mipaka ya Bongo kwa kuliona hilo wameamua kuarika wasanii mbalimbali kwa ajili ya kuzindua filamu hiyo ambayo inasemekana kuwa ni kazi ya kipekee.

“Tunatarajia kufanya tukio la kipekee kabisa katika uzinduzi wa filamu ya Love and Power ya marehemu Kanumba kwa sababu ni mtu wa watu kwa hiyo kutokana na habari tumekuwa tukizipata kutoka sehemu mbalimbali kuna watu ambao bado hawaamini kuwa Kanumba yupo hai, katika kumuenzi tumekusudia kuitendea haki filamu yake,”anasema Mwanyilu.

Filamu ya Love and Power ni filamu ambayo inasubiriwa kwa hamu na wapenzi wa filamu kutokana na kile kilichowahi kusikika kuwa filamu hiyo ilitabri kifo cha marehemu Kanumba, katika filamu hiyo pia wapo wasanii kama Irene Paul, Patcho Mwamba, marehemu Sharomilionea na wasanii wengine wengi
CHANZO:FILAMU CENTRAL


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo