BIFU LA LADY JAY DEE, BEN PAUL NA LINNAH

ben-pol-linah-sanga-lady-jaydee-judith-wambura
Wengi wenu mnafahamu kwamba hivi karibuni Lady Jaydee aliwachana Clouds FM kwa kupitia Twitter na kudai wanarusha nyimbo za wasanii wao tu hewani. 

Kwa msiofahamu, tweet ifuatayo ndiyo iliyoanzisha hii saga: “Radio ya watu isiopiga nyimbo za wasanii wa watu ila za wasanii wao tu, wasiopendwa na watu. #JotoHasira”

Treni la Jaydee la kuwashukia watu linaonekana kuendelea bila kupunguza kasi, maana masaa kadhaa yaliyopita, aliamua kuwashukia wasanii wa THT, Linah na Ben Pol. Zifuatazo ni kauli za Jaydee kupitia Twitter, na majibu ya Ben Pol:

Lady JayDee – Wasanii wa THT walikatazwa kuja kuimba Nyumbani Lounge siku ya Valentine na boss wao. Mbali na kuwa walishalipwa hela za advance
Lady JayDee – Linah na Ben Pol mnabisha hamkukatazwa? Nisalitini ila hamtapata faida mtatoka kapa pia.

Lady JayDee – Walidhani ni show yangu, wakafikiri nitatajirika. Ila nilitoa ukumbi tu wakamsaliti alieandaa show. Not me
Majibu ya Ben Pol:

Ben Pol – @JideJaydee Don’t talk about things your don’t know about. DON’T.
Ben Pol – @JideJaydee hiyo show kulikuwa na wengine pia wakuperform je wali perform? kama nililipwa nanikashindwa ku show up, mbona sidaiwi?? Tafakari



JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo