ZAIDI YA MILIONI 21 KUTUMIKA KUINUA ELIMU MIRERANI

 
Zaidi ya kiasi cha shilingi milioni 21.658 zimefanikiwa kukusanywa za mfuko wa elimu kwa mwaka jana ambazo zimetumika kuinua elimu katika kata  ya Endiamtu iliyopo Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara
 
 Taarifa hiyo imetolewa na Ofisa mtendaji wa kata hiyo,Edmund Tibiita  wakati akiongea  kwenye kikao cha maendeleo cha kata hiyo (WDC)  ambapo alieleza kuwa  fedha hizo zilichangwa na wananchi mbalimbali wa vitongoji vinne vinavyounda kata hiyo.
 
 Aidha alisema kuwa  kitongoji cha Kazamoyo walichanga shilingi milioni 8.3 ,Zaire walichanga shilingi milioni 2.7,Kairo walichanga shilingi 750,000,kitongoji cha Sekondari walichanga shilingi milioni 2 na kitongoji cha Kilimahewa walikusanya shilingi milioni 2. 
 
 Pia aliongeza kuwa  askari polisi wakiongozwa na mkuu wa kituo cha polisi Mirerani ASP Ally Mkalipa,walitoa sh310,000 Diwani wa kata ya Endiamtu,Lucas Zacharia alijitolea sh3 milioni na wamiliki wa magari ya DCM walijitolea sh360,000.
 
 Alisema kuwa wengine waliowachangia ni marafiki wa Diwani wao Lucas waliojitolea shilingi milioni 2 ,wafanyabiashara wa maduka shilingi 830,000  pamoja na vifaa vilivyobambuliwa vina thamani ya shilingi 375,000.
 
 Kwa upande wake Diwani wa kata ya Endiamtu Lucas Zacharia,amewataka  wazazi pamoja na  walezi wa kata  hiyo  kutoa kipaumbele pamoja na kuzingatia kwa  kuwapatia watoto wao elimu kwani kwa dunia ya sasa bila kuwa na elimu Taifa litakuwa gizani. 
 
 “Jamani Elimu iwe ndiyo ajenda yetu ya kwanza kwa sisi kata ya Endiamtu hivyo tujitahidi kwa kadiri ya uwezo wetu katika kuhakikisha kuwa watoto wetu wanapata elimu bora na iliyo katika mazingira mazuri,” alisisitiza Zacharia.
 
 Aliendelea kusema kuwa hivi sasa wanatakiwa kuweka nguvu moja kwenye ujenzi wa madarasa ya shule mpya ya msingi Zaire na Endiamtu,kwani shule za msingi Mirerani na Jitegemee hazina maeneo ya kujengewa madarasa mapya.
 
 Amewaasa  wajumbe wa kamati ya maendeleo ya kata hiyo (WDC) wajitolee kwa moyo mmoja,katika kuhakikisha kuwa wanawatumikia ipasavyo wananchi waliowachagua kwani huu siyo wakati wa kufanya siasa.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo