SERIKALI YATAKIWA KUWEZESHA UJENZI WA MABWENI KWENYE SEKONDARI HASA VIJIJINI

SERIKALI imeombwa  kuwezesha ujenzi wa mabweni kwenye shule za sekondari hasa zilizopo vijijini kwani ukosefu wa mabweni huchangia kwa kiasi kikubwa kwa wanafunzi wa kike kupata ujauzito  pamoja na kukatiza masomo.
Ombi hilo limetolewa mwanafunzi wa kidato cha tatu wa shule ya sekondari ya Chief Gijaru John wakati akichangia kwenye mdahalo wa wananchi wa jinsia na maendeleo ulioandaliwa na Mtandao wa asasi za kiraia Mkoani Manyara (Macsnet) na  kufanyika katika kijiji cha Balang’dalalu Wilayani Hanang’ mkoani Manyara.
Alisema kuwa  endapo Serikali ingeliweka kipaumbele kwa kujenga mabweni mashuleni hasa vijijini,wasichana wangesoma vizuri bila kurubuniwa kama ilivyo hivi sasa ambapo baadhi yao hupewa ujauzito na kukatisha masomo yao na ukosefu wa mabweni ndiyo chanzo cha upatikanaji wa mimba kwa wanafunzi wa kike.
Kwa upande wake mmoja wa washiriki hao ambaye ni mjasiriamali Mary Gitagno amewataka  wasichana  kuzingatia masomo ambayo ndiyo yatakayowakomboa kwenye maisha yao yajayo na wasikubali kurubuniwa na wanaume ili hali bado wanaendelea na masomo yao.
Aidha aliongeza kuwa  yeye ni mzaliwa wa kijiji cha Bassotu wilayani humo ambaye alipata elimu yake mjini Moshi mkoani Kilimanjaro ambapo  wanaume walijaribu kumrubuni kipindi hicho akisoma lakini walishindwa kumpata.
Amewaasa wanafunzi hao wasikubali kuhadaika na kudanganywa na mwanaume wakidai kuwa eti wao ni my moyo,kidege changu,yeye ni nyota yake!kisha unakubali kurubunika, hivyo wasome na wasiingie huko.
Pia kutokana na shule nyingi za sekondari kukosa mabweni wanafunzi wengi wa kike wanapangisha vyumba vijijini huku wakiendelea na masomo yao shuleni hivyo kuwafanya warubuniwe na wanaume kwa urahisi zaidi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo