DC RUNGWE AFANIKIWA KUMALIZA MGOGORO WA MAJI


Na Ibrahim Yassin,Rungwe

MKUU wa wilaya Rungwe mkoani Mbeya Chrispini Meela amefanikiwa kuumaliza mgogoro wa maji uliodumu kwa muda wa mwaka mmoja sasa kati ya Wanananchi na mamlaka yamaji safi na taka mjini Tukuyu (TUWSA)

Mgogoro huo ulianza Agosti 8 mwaka wa 2011 ambapo mamlaka ya maji mjini Tukuyu ilipowatangazia wateja kupanda kwa gharama za maji kutoka sh,2000 hadi 4500 na watumiaji kufungiwa nira ambapo watumiaji hao wa maji hawakuridhia hari hiyo na kupeleka malalamiko yao kwa aliyekuwa mkuu wa wilaya hiyo kipindi hicho Bw,Jacson Msome

Licha ya malalamiko yao kupelekwa kwa mkuu wa wilaya hawakuweza kufikia ufumbuzi wa tatizo hilo ambapo watumiaji hoja yao kubwa ilikuwa kwamba hawaoni sababu za kupanda bei za maji wakati miundo mbinu ya maji ni ileile ya zamani na michakavu hakuna kilichoongezeka hivyo hawaoni sababu ya msingi ya ongezeko hilo na kuamua kuunda umoja wa watumiaji maji wa kata saba(MBIKI) chini ya mwenyekiti wake Watson Mwakanyamale

Mvutano huo ulikuja kuwa mkubwa na kuamua kumshirikisha mbunge wa  jimbo hilo Prof,David Mwakyusa  ambapo naye aliungana na mamlaka ya maji ya mjini Tukuyu juu upandaji wa bei na ufungaji nira ambapo watumiaji maji hao wa maji waliamua kupeleka malalamiko yao mahakamani  ambako kesi iliendelea hadi jana serikali ya wilaya ilipoamua kuwekeana saini mbele ya Wakili Mkumbe kuwa kesi iliyopo mahakamani ifutwe na waendelee kulipia maji  kwa bei y ash,2000 wote wenye nira na wasio na nira

Akitia saini ya makubaliano hayo mkuu huyo wa wilaya mbele ya umati mkubwa wa Wananchi ambao ndiyo watumiaji wa maji alisema kuwa haoni sababu za kuendelea na malumbano bali kesi iliyopo mahakamani ifutwe na wananchi waendelee kuchangia kiasi hicho cha fedha ili mamlaka hiyo iendelee kufanya kazi kuliko hari ilivyo hivi sasa ambapo mamlaka hiyo haikusanyi chochote kutoka kwa watumiaji maji hasa baada ya kesi hiyo kwenda mahakamani

Alisema kwa hari hiyo sasa watumiaji wa maji sasa wamefutiwa madeni yao yote waliyokuwa wakidaiwa wakati wa mgogoro huo wote na kuwa hata hiyo bili ya maji y ash,2000 itaanzwa kutozwa mwezi machi mwaka huu  na kuwa mkataba huo utakuwa ndani ya matazamio kwa muda wa miezi mitatu kuanzia mwezi ujao

Ukumbi wa hospitali ya wilaya Rungwe jana ulizizima kwa furaha baada ya wananchi waliohudhuria mkutano huo kuonyesha furaha kubwa huku wakimpongeza  mkuu huyo wa wilaya kwa kuweza kuumaliza mgogoro huo vizuri kabisa wakati viongozi waliomtangulia walishindwa kuutafutia ufumbuzi na kumuona kama mfalme


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo