WAFUGAJI WAONYWA KUPELEKA MIFUGO YAO MAENEO YALIYOTENGWA KWA AJILI YA UFUGAJI NYUKI

Mkuu wa wilaya ya Babati Khalid Mandia amewataka wafugaji kutokupeleka mifugo yao katika maeneo yaliyotengwa kwaajili ya ufugaji wa nyuki. 
 
Rai hiyo ameitoa siku ya ugawaji wa mizinga mradi pacha wa ufugaji nyuki Mwikantsi kata ya Mamire wilayani  Babati mkoani Manyara. 
 
Alisema kuwa maeneo hayo yaepukwe kukata miti ovyo pamoja na kuendesha shughuli za kilimo pamoja na kuchoma ili ufugaji wa nyuki uweze kuwa wa tija.
Aliongeza kuwa katika ufugaji wa kisasa mizinga inapaswa itengenezewe vichanja vya urefu wa kufika kiunoni kutoka usawa wa ardhi kufanya shughuli za  ukaguzi uvunaji wa asali na mengineyo kuwa rahisi na usihitaji watu wengi kufanya. 
 
Aidha aliendelea kusema kuwa serikali ya kijiji kwa kushirikiana na wanakijiji waweke utaratibu madhubuti wa kulinda mazingira kwa faida yao pamoja na watoto wao. 
 
Mkuu wa wilaya huyo Khalid amesikitishwa sana na taarifa wanazozipata kutoka TANAPA  Tarangire na ofisi ya mtendaji wa kijiji kumekuwa na wimbi kubwa la wananchi wanaovamia eneo la hifadhi kwa kuchungia mifugo na kukata miti hovyo. 
 
Alisema kuwa maeneo ya hifadhi ni marufuku kufanya shughuli yeyote wakiendelea kufanya hivyo kizazi kijacho kitabaki kuona mashamba na mifugo badala ya wanyama pori kwani wanyama wanaposumbuliwa wanakimbilia hifadhi jirani na hatimaye wanatokomea nchi jirani. 
 
‘’Hifadhi hii inafaida nyingi kwetu ikiwa ni pamoja na huduma tunazopata moja kwa moja hapa kijijini kama shule na kuchangia pato la Taifa ,serikali ya kijiji pamoja na wananchi tuwe mstari wa mbele katika kulinda na kutunza rasilimali zetu.Alisema Mkuu wa wilaya Khalid.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo