WANACHAMA WA CCM WATISHIA KUKIHAMA CHAMA HICHO

Inasemekana kuwa wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Kijiji cha Shambarai Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara wametishia kuhama chama hicho kutokana na  baadhi ya viongozi wa kijiji hicho kudaiwa kuuza maeneo ya wazi bila utaratibu. 
 
Taarifa hiyo imetolewa na na baadhi ya wanachama hao ambao hawakutaka kutaja majina yao  kutaja majina yaowakati wakiongea  na waandishi wa habari ambapo alibainisha kuwa wamefikisha kilio chao kwa uongozi wa CCM wa kata hiyo kwa kuwa wametokana na chama hicho lakini hakuna hatua zilizochukuliwa. 
 
Aidha alisema kuwa  mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji hicho,Edward Wazi na Ofisa Mtendaji wa kijiji hicho,Mosses Peter wamewauzia mashamba matajiri kutoka Arusha bila kufuata utaratibu wa kuidhinishwa na mkutano wa kijiji. 
 
Waliendelea kusema kuwa  viongozi hao wamefunga maeneo ya kijiji chao ikiwemo mapalio ya kupitishia mifugo na wakihoji kwa viongozi hao kwa nini wameuza maeneo yao wanatishiwa kwa maneno hivyo wanashindwa mahali pakwenda.
 
Walisema kuwa wamefikisha suala hilo hadi kwenye ofisi ya CCM ya kata kwani viongozi hawa wametokana na CCM lakini hakuna hatua zozote zilizochukuliwa dhidi yao.
 
Pia alieleza kuwa  mashamba hayo yaliyouzwa yaliachwa tangu mwaka 1975 kwa ajili ya maeneo ya kulishia mifugo lakini wameshangazwa na viongozi hao kuamua kuyauza kwa wafanyabiashara hao kutoka mkoani Arusha.
 
Kwa upande wao mwenyekiti wa kijiji cha Shambarai Edward Wazi na Ofisa Mtendaji wa kijiji hicho,Mosses Peter wamekanusha vikali kuuza maeneo hayo ila walidai kuwa yameuzwa na wamiliki husika wa maeneo hayo.
 
Walisema  kuwa maeneo hayo siyo ya Serikali ila wamiliki wenyewe wameyauza mashamba hayo ambayo ni mali yao na wao hawana mamlaka ya kuingilia au kutoa uamuzi juu ya mashamba hayo.
 
Walisisitiza kuwa  wamiliki hao wameyauza kihalali mashamba hayo baada ya kupata shida kwani kimfaacho mtu ni chake hivyo hawana uamuzi wa kumzuia kuuza kwani wenyewe hawamiliki chochote na wala hawahusiki na mashamba hayo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo