HALMASHAURI KUTUMIA ZAIDI YA BILIONI 33 KWA AJILI YA MISHAHARA NA MENGINEYO

Imebainishwa kuwa  makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2013- 2014 Halmashauri ya wilaya ya Babati mkoani Manyara inatarajia kutumia kiasi cha shilingi bilioni 33,323,868,975.00 kwamwaka wa fedha kwaajili ya kulipa mishahara ya watumishi,matumizi mengineo na kugharimia miradi mbali mbali ya maendeleo.
Hayo yamebainishwa na mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Babati Dominic Kweka wakati akisoma taarifa ya mapato  na matumizi ya mwaka 2013-2014 kwenye kikao cha baraza la madiwani  halmashauri ya wilaya ya babati kilichofanyika Halmashaurini hapo mkoani Manyara.
Alibainisha kuwa  kati ya fedha hizo  kiasi cha shilingi bilioni 21,333,087,772,00  ni mapato ya vyanzo vya ndani,ruzuku ya matumizi mengineo(oc),mishahara ya watumishi na kiasi cha shilingi  bilioni 11,990,781,185.00 ni fedha za miradi ya maendeleo mbalimbali.
Pia alitaja aina ya miradi hiyo kuwa ni mradi wa kilimo,mradi wa ukimwi,mradi wa barabara,mfuko wa kujenga uwezo(cbg),miradi ya maendeleo(cdg),mpango wa maendeleo ya afya ya msingi,mfuko wa afya,mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi na sekondari,mradi wa maji vijijini,miradi ya jamii,wadau wa maendeleo world vision/wahisani wengine pamoja na michango ya wananchi.
Alisema kuwa  kwa upande wa matumizi Halmashauri hiyo inatarajia kutumia kiasi cha shilingi bilioni 33,190,838,510.00 kwa mwaka wa fedha 2013-2014 kwaajili ya  kulipa mishahara ya watumishi,matumizi mengineo na kugharimu miradi mbalimbali ya maendeleo.
Aliendelea kusema kuwa  hadi mwezi disemba 2012 matumizi yote ni kiasi cha shilingi 10,195,790,0112.20 kati ya fedha hizi ni shilingi  bilioni 1,214,250,276 ni matumizi ya bakaa ya mwaka 2011-2012 na shilingi bilioni 8,981,539,735.00 ni matumizi ya bajeti ya mwaka 2011-2013 ambayo ni sawa na asilimia 39% ya lengo ambapo katika maeneo ya matumizi kuwa ni vyanzo vya ndani vya Halamashauri,matumizi mengineo,mishahara,mfuko wa barabara,ukarabati wa kituo cha wazee Sarame pamoja na mfuko wa  jimbo
Mkurugenzi Kweka alitaja changamoto zilizojitokeza katika utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2012- 2013 kutokuwepo kwa mvua za kutosha kulisababisha mavuno ya mazao ya kilimo kupungua na hivyo kuathiri ukusanyaji wa ushuru wa mazao,baadhi ya vijiji kutokuwepo na watendaji hivyo usimamizi na utekelezaji wa shughuli za maendeleo kukwama.
Vile vile aliendelea kutaja changamoto zingine kuwa ni  ruzuku kutoka serikali kuu kutokufika kwa wakati au hata kutokuletwa kabisa hivyo kukwamisha utekelezaji wa miradi iliyokusudiwa,mfumuko mkubwa wa bei ambao umesababisha gharama  huduma na bidhaa mbalimbali kupanda maradufu kama mafuta,umeme,maji,vipuri n.k.
Alisema kuwa mikakati ya kukabiliana na changamoto  zilizojitokeza katika utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2012-2013 ni kujaza  nafasi  wazi za watendaji wa vijiji,kuboresha idara ya fedha kwa kuomba ongezeko la wahasibu pamoja na maafisa biashara pia kuongeza jhudi katika ukusanyaji wa mapato hasa katika eneo la viwanda na kambi za kitalii na kuendelea kufuatilia na kuikumbusha serikali  umuhimu wa kutoa fedha za miradi ya maendeleo kwa wakati.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo