WANASAYANSI WABAINI KUWA INAWEZEKANA KUONDOA MAAMBUKIZI YA VVU


Wanasayansi wamebaini kuwa inawezekana kuondoa maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto (EMCTC) tofauti na ilivyozoeka kuwa ni kupunguza maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto(PMCTC)

Pia malengo, mipango na mikakati ilivyowekwa na wadau mbalimbali wanaohusika na mapambano dhidi ya virusi vya UKIMWI ikifuatwa na kutumiwa ipasavyo ndiyo njia pekee itakayowezesha kuondoa maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto

Akizungumza kwenye kikao cha wadau mbalimbali kilichofanyika kwenye ukumbi wa hospitali ya wilaya Makete Dkt. Rugola Mtandu, (CEO, PHARMKONSULT AFRICA LTD) amesema mpango huo unatekelezwa kwenye nchi 42 duniani ambazo zina maambukizi makubwa ya virusi vya UKIMWI ikiwemo Tanzania

Amesema inawezekana kuondoa maambukizi hayo kwa asilimia 90 na pia kuhakikisha kina mama nao wanazidi kuwa hai, na unatekelezwa kwa wanawake waliopo katika uwezo wa kubeba mimba, miaka 15-49

Ameyataja malengo makubwa ya kuondoa maambukizi ya mama kwenda kwa mtoto kuwa ni kupunguza maambukizi hayo hadi kuwa chini ya asilimia 5, kupunguza kwa asilimia 90 ya maambukizi mapya ya vvu kwa akina mama na wao wawe hai,njia za uzazi wa mpango zipatikane kwa wanawake wote, pamoja na upatikanaji kwa asilimia 90 wa ART kwa wajawazito ambao wana vvu

Wilaya ya Makete ni miongoni mwa wilaya zilizopo hapa nchini ambazo zina maambukizi ya virusi vya ukimwi hivyo jitihada mbalimbali zimekuwa zikichukuliwa na serikali na mashirika yasiyo ya kiserikali pamoja na wananchi kupambana na changamoto hiyo




JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo