MOSHI
VIJANA
zaidi
ya 30 katika kata ya Kahe wilaya ya Moshi vijijini mkoani
Kilimanjaro wamenufaika na mafunzo ya ujasiria mali ikiwa ni pamoja na
kujiajiri wenyewe katika shughuli za kilimo kutokana kuwepo kwa
changamoto ya ukosefu wa ajira nchini.
Hayo
yalibainishwa na mkurugenzi mtendaji wa shirika lisilo la kiserikali la
kuwawezesha vijana kujiajiri katika kilimo na ujasiriamali ili kupambana
na
tatizo la ajira kwa vijana la 'Fumbuka Agro Solution Organization
(FASO)'
Innocent Mbele ambapo alisema vijana wengi wamekuwa hawana ajira na
kujikuta
wakiingia katika makundi ya uvutaji wa madawa ya kulevya jambo ambalo
limekuwa
likipoteza nguvu kazi ya taifa.
Alisema
kutokana
na vijana wengi kukosa ajari shirika hilo limeoana ni vema kutoa elimu
ya ujasirimali kwa vijana kuhusiana na kilimo kutokana na kwamba ndilo
kundi
kubwa linalo kabiliwa na changamoto ya ukosefu wa ajira.
Alisema
vijana
wengi ni wasomi lakini wamekuwa wakishinda vijiweni na hatimae kujikuta
wanakuwa vibaka na kwamba kwa kutoa elimu hiyo ndio njia pekee ya
kuwawezesha
vijana na kwamba hawana budi kubadilisha fikra za kuajiriwa bali
kujiajiri
wenyewe ili kuondokana na tatizo la umasikini wa kipato
Kwa
upande wake Diwani wa kata ya Kahe, Aminiel Kimati alitoa wito
vijana kufanya kazi kwa bidii na kwa na subira kutokana na kamba
maendeleo haji kwa hara bali kujituma na kuwa na maadili katika jamii
ikiwa ni
pamoja na kuacha tabia ya utumiaji wa madawa ya kulevya.
Mkufunzi
wa semina hiyo Mwl.Simon Mushi kutoka chuo cha Kilimo na Mifugo
Mwangaria
aliwafundisha vijana hao jinsi ya kuchagua mazao bora kulingana na hali
ya hewa
ya ukanda wao pia jinsi ya kuchagua pembejeo bora za kilimo kama mbegu,
mbolea
na madawa ya kuuwa wadudu.