Simanjiro.
WAAMINI wa Kanisa
Katoliki Parokia
ya Bikira Maria Malkia wa Rozali wa Mji mdogo wa Mirerani Wilaya ya
Simanjiro
Mkoani Manyara wamempa zawadi ya gari padri Gasto Sinkala ambaye amepata
upadri
hivi karibuni mjini Arusha.
Taarifa hiyo imetolewa na mwenyekiti
wa kamati ya misa hiyo,Nobert Olomi wakati akiongea na waandishi wa
habari baada ya misa ya shukrani ya kupata upadri iliyofanyika kwenye
Parokia ya Mirerani wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara.
Aidha mwenyekiti huyo wa kamati ya
misa hiyo,Nobert Olomi alisema kuwa gari hilo aina ya Suzuki Escudo lina
thamani ya sh11 milioni.
Aliongeza kuwa waamini wameona
wampe zawadi ya gari hilo ili kumrahisishia usafiri padri Sinkala kwenye
eneo
lake la uinjilishaji huko Loliondo na pia awakumbuke waamini wa Mirerani
kwa
sala kila akilitumia gari hilo.
Aidha akitoa shukrani kwa waamini wa
kanisa hilo wakiongozwa na mapadri wa Jimbo Kuu Katoliki Arusha,Pastory
Kijuu,Aloyce Kitomari,Raphael Loratare na Theopil Mroso,Padri Sinkala
alisema
anamshukuru Mungu kwa kufanikisha wito wake.
Padri Sinkala alibainisha kuwa
japokuwa amelelewa katika mazingira na mikono ya watu tofauti wakiwemo
wazazi na ndugu zake hatimaye amefanikiwa kupata daraja la upadri ambalo
alikuwa na wito nao tangu akiwa mdogo.
“Jamani namshukuru Mungu hata
kunifikisha hapa leo ingawa wazazi wangu wapo hai lakini hivi sasa wapo
nyumbani Mbeya hawajashuhudia umati huu uliopo leo hii lakini furaha
yangu na
yenu ndiyo furaha yao pia,” alisema Padri Sinkala.
Naye Padri Mroso ambaye ni mlezi
wa imani wa Padri Sinkala alieleza kuwa waamini wa Mirerani wameweka
rekodi kwa kununulia gari ambalo litamsaidia Padri huyo kwenye
uinjilishaji.
“Mirerani mpo juu kwani katika historia
ya Jimbo Katoliki la Arusha hakuna padri aliyepewa gari na waamini ninyi
ni wa
kwanza nadhani vijana wa Mirerani miaka ijayo wakipata upadri mtawapa
helkopta
au ndege,” alisisitiza Padri Mroso
Kwa upande wake Padri Pastory Kijuu
aliyekuwa Paroko wa Kanisa Katoliki Mirerani na ambaye anasoma chuo
kikuu cha
Nairobi alifafanua kuwa kila shughuli za kichungaji atakayofanya Padri
Sinkala watu wa Mirerani watabarikiwa.
“Mimi nilipoanza upadri mwaka 1981
nilikuwa natumia baiskeli hivyo nawapongeza kwa kumtunza gari Padri
Sinkala
japokuwa hata asingepata hilo gari angetoa huduma ya upadri bila
matatizo,”
alisema Padri Kitomari.
Paroko mpya wa Kanisa Katoliki
Mirerani,AlouKitomari alifurahishwa na kitendo cha waamini hao kumpa
gari Padri
Sinkala kupewa gari ambalo litamsaidia kufanya uinjilishaji huko
Loliondo,Dikodiko na Samunge wilayani Ngorongoro.
