UKOSEFU WA MITAMBO YA SIMU KATIKA VIJIJI BADO NI CHANGAMOTO KWA SERIKALI

Serikali imesema inakamilisha sehemu muhimu ya maeneo ya msingi kwa ajili ya utekelezaji wa mpango wa taifa wa kufikisha mawasiliano ya simu katika vijiji vyote hapa nchini

Taarifa hiyo imetolewa na waziri wa fedha Dkt. Wilium Mgimwa kwa waandishi wa habari katika kijiji cha Kidamali Mkoani Iringa baada ya mkutano wa hadhara baada ya wavijiji katika wilaya ya Iringa vijijini kutaka serikali imalize kero ya kukosa simu za kiganjani

Dkt. Mgimwa amesema serikali inaendelea kutafuta mkandarasi wa kufanya uchambuzi ili kuona namna serikali itakavyoshirikiana na wawekezaji kufanikisha utekelezaji wa mpango huo wa kusambaza huduma za simu kila sehemu nchini

Katika mikutano hiyo wananchi wa viijiji hivyo walidai huduma hiyo ya simu za mkononi ni ya muhimu kwa sasa hivyo serikali inatakiwa kuharakisha

Katika kijiji cha Ikungwe na kijiji cha Mfyambe pia wakazi hao hawakusita kutoa kero zao ambao pia zilijibiwa na Mh. Waziri ikiwemo ulanguzi wa pembejeo za kilimo hasa mbolea za ruzuku


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo