JESHI LA POLISI MKOANI KATAVI LAKAMATA JANGILI MMOJA


Jeshi la polisi mkoani Katavi kwa kushirikiana na askari wa TANAPA katika hifadhi ya Katavi imefanikiwa kumkamata jangili Jonathan Charles mkazi wa Ulwila akiwa na silaha moja ya kivita aina ya smg ikiwa na risasi 30 ndani yake

Akizungumza na waandishi wa habari kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Katavi Joseph Myovela amesema poaresheni hiyo ilifanyika katika eneo la Ilumbi ndani ya hifadhi ya taifa wilaya ya Mpanda kwa lengo la kuwasaka wawindaji haramu wenye silaha za kivita nab ado jeshi hilo linawasaka watu watatu

Amesema bunduki hiyo iliyokamatwa ni namba M22/13350 ambapo kukamatwa kwa mtuhumiwa huo kumetokana na mtego uliowekwa ambapo baada ya kuzingirwa majangili hao walianza kufyatua risasi hali iliyopelekea kukamatwa kwa mtuhumiwa mmoja


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo