BOMU LILILOKUTWA LIKICHEZEWA NA WATOTO MKOANI MTWARA LAHARIBIWA NA JWTZ NA POLISI

Jeshi la polisi mkoani Mtwara kwa kushirikiana na jeshi la wananchi wa Tanzania wamefanikiwa kuharibu  bomu lililokuwa limetelekezwa katika kijiji cha Mdui kata ya Mbawala wilaya ya Mtwara vijijini baada ya kuonekana likichezewa na watoto. 

Akizungumza na vyombo vya habari kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Mtwara Maisha Maganga amesema taarifa hizo wamezipata kutoka kwa raia wema baada ya kuonekana likiwa eneo la makaburi.

Amesema baada ya kupata taarifa juu ya bomu hilo lenye kilo nne jeshi hilo lilichukua hatua za haraka ikiwa ni pamoja na kuomba kikosi maalum cha kutegua mabomu kutoka jeshi la wananchi wa Tanzania.

Amesema bomu hilo linaonyesha ni la siku nyingi mahali hapo na  liliachwa enzi za vita ya Msumbiji.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo