WATAKAOHAMASISHA WANANCHI WASISHIRIKI SENSA KUKIONA CHA MOTO


                                  RC MAHIZA

Mkuu wa mkoa wa Pwani Mh. Mwantumu Mahiza amesema mkoa wake utawachukulia hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kuwakamata na kuwafikisha mahakamani watu wote wanaowahamasisha wakazi wa mkoa huo  kutoshiriki katika sensa ya watu na makazi itakayofanyika Agosti 26, mwaka huu

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mahiza amesema imefikia hatua hiyo kutokana na kuwepo kwa baadhi ya makundi ya watu ambao wanahamasisha wananchi kususia kushiriki katika zoezi la sensa kwa kisingizio cha dini na kisingizio cha korosho kukosa soko

Katika taarifa yake aliyoitoa kwa waandishi wa habari amesema endapo itatokea mtu ama kikundi cha watua ambacho kitazuia familia yeyote isitoe taarifa wakati wa sensa ya watu na makazi atakuwa amefanya kosa la jinai hivyo ni lazima achukuliwe hatua za kisheria


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo