SENSA BADO INAENDELEA VIZURI MARA

 
ZOEZI la Sensa na Makazi mkoani Mara  linaendelea Vizuri mpaka sasa licha ya kuwepo kwa kasoro ndogo tangu kuanza kwake hapo Siku ya Jumamosi usiku chini nzima.
 
Mratibu wa Takwimu mkoani Mara Bw. Ramadhani Mbega amesema kuwa mpaka sasa taarifa alizozipata kutoka sehemu mbalimbali mkoani Mara zinaashiria zoezi hilo kwenda vizuri.
 
Amesema Matatizo madogo ambayo yalikuwepo kama vifaa,picha kwa makarani kama utambulisho yametatuliwa na hivyo zoezi zima kuendelea kama lilivyopangwa.
 
Aidha katika maeneo ya Mbugani na Visiwani,Bw Mbega amesema kuwa zoezi hilo limeendelea Vizuri kutokana na maandalizi yaliyokuwe hapo awali.
 
Mbali na maeneo hao Bw. Mbega amesema kuwa kuna baadhi ya maeneo ambapo viongozi wa vijiji na vitongoji walikuwa wanalalamika juu ya maalipo yao na kuongeza kuwa malipo hayo yanatolewa kwa awamu kama ilivyoagizwa
 
Kwa sababu hiyo Mratibu huyo wa Takwimu mkoa wa Mara amewataka wananchi wote wa Mkoa wa Maraa kuendelea kujitokeza katika zoezi hilo kwani kwa kufanya hivyo wataisaidia Serikali katika kupango mipango ya Maendeleo kwa wananchi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo