NOTI BANDIA ZAKAMATWA IRINGA

Noti bandia zatua Iringa
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Iringa Michael Kamuhanda akionyesha mfano wa noti za shilingi 10000 ambazo ni feki zilizokamatwa na jeshi la polisi zikiwa na thamani inayofanana na Tsh. zaidi ya 700,000
Jeshi la polisi mkoa wa Iringa limetoa tahadhari kwa wananchi kuwa makani na fedha wanazolipwa ili kuepuka kubambikizwa noti bandia ambazo tayari jeshi hilo limekamata zaidi ya bandia zenye thamani ya zaidi ya shilingi 700,000.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Iringa Michael Kamuhanda amesema leo kuwa noti hizo zimekamatwa na askari polisi baada ya kupata taarifa kutoka kwa wananchi wasamaria wema.

Kamuhanda alisema kuwa hadi sasa jeshi hilo la polisi linawasaka wahusika wa mtandao huo wa kusambaza noti bandia katika mkoa wa Iringa ili kuchukuliwa hatua za kisheria.

Alisema kuwa fedha hizo ambazo zimekamatwa katika maeneo tofauti tofauti zina namba ambazo zinafanana na hivyo kuwataka wafanyabiashara na wakulima kuwa makini na watu wanaofika kununua mazao yao 

HABARI KWA HISANI YA www.francisgodwin.blogspot.com.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo