CHADEMA MAKETE YAWATAKA WANANCHI KUSHIRIKI SENSA YA WATU NA MAKAZI WILAYANI HUMO


MAKETE

Chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) wilayani Makete kimewataka wananchi wote kushiriki kikamilifu katika sensa ya watu na makazi inayotarajiwa kufanyika usiku wa kuamkia Agosti 26 mwaka huu

Akizungumza na mwandishi wetu Mwenyekiti wa CHADEMA wilaya ya Makete Shaaban Mkakanze amesema suala la sensa halina itikadi za vyama bali ni kwa maendeleo ya taifa hivyo wananchi wajitikeze kuhesabiwa

“Sisi kama CHADEMA hatuna ubishi wala hatukatazi watu kushiriki katika sensa, tunahimiza watu wote wajitokeze kushiriki sensa, na hata sisi kwenye mikutano yetu ya hadhara hapa Makete tunawahimiza wananchi wote wajitokeze kwa wingi katika sensa” alisema

Katika hatua nyingine Mwenyekiti huyo amewashukuru wananchi waliotoa michango yao kufanikisha mikutano waliyoifanya katika tarafa ya Ikuwo, na kuwaomba wananchi wenye mapenzi mema na chama hicho kuendelea kutoa michango yao ikiwa ni pamoja na kukisaidia kushiriki wa mgombea wa chama hicho katika uchaguzi wa diwani wa kata ya Luvumbu wilayani hapo

Amesema michango ya wananchi hao itatangazwa kwenye vyombo vya habari lakini kama yupo aliyetoa michango na hataki itangazwe wao kama CHADEMA watazingatia hilo, hivyo kusema chama hicho hakina ubaya na mtu bali kinaipa changamoto serikali iliyopo madarakani ili ijisahihishe kutokana na changamoto zinazoikabili


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo