Tyson Nduguru rafiki wa marehemu MC Joe aliyepotea, apatikana

Kijana Tyson Nduguru, Rafiki wa karibu wa Joel Misesemo (MC Joel) aliyejirusha ghorofa ya 7 Makumbusho Dar es salaam na kufariki dunia, ambaye aliripotiwa kutoweka ghafla siku tatu tangu kutokea kwa kifo cha Joel, amepatikana jana June 1 2023.


Mke wa Tyson, Grace Rashid ameithibitisha kwa kusema; “Ni kweli Tyson amepatikana mchana wa leo (jana), mimi nilitoka kama kawaida nilikua naendelea na mizunguko akanipigia simu yeye mwenyewe.

“Nimefika nyumbani nimeshaonana nae ni mzima wa afya, mpaka sasa sijaongea nae lolote Watu wapo wengi tupo na familia, nitawajulisha zaidi baadae."

Ripoti za kutoweka kwa Tyson ziliibua maswali mengi kutokana na ukaribu wa wawili hao pamoja na matukio mawili tofauti yaliyowatokea kwa kupishana siku chache yakiwa na mazingira ya kutatanisha.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo