Nyama ya Nguruwe yaruhusiwa kwa masharti Ludewa

Baada ya kutolewa katazo la kutumia mazao yatokanayo na mnyama aina ya Nguruwe wilayani Ludewa mkoani Njombe ambalo lilitolewa kwa zaidi ya miezi miwili na nusu iliyopita kwa kile kilichodaiwa ni kutokana na uwepo wa ugonjwa wa homa ya Nguruwe hatimaye mnyama huyo ameweza kupunguziwa masharti ya katazo hilo baada ya kupungua kwa matukio ya ugonjwa huo.


Akizungumza na Wasafi media Afisa Kilimo Mifugo na Uvuvi Festo Mkomba amesema mnyama huyo ameruhusiwa kuchinjwa pamoja na kutumika mazao yake kama nyama, mifupa, nywele, samadi na damu ila hairuhusiwi kutoa mazao hayo nje ya kijiji ambacho mnyama huyo amechinjwa ambapo na kabla ya kuchinjwa kwake anatakiwa kufanyiwa ukaguzi kwa masaa yasiyopungua 48.

Ameongeza kuwa mpaka sasa zaidi ya nguruwe 417 wamekufa kwa ugonjwa huo na wamefanya jitihada za kutosha kuhakikisha ugonjwa huo hauenei zaidi na wamefanikiwa ambapo kwa sasa hakuna nguruwe hata mmoja mwenye ugonjwa.

"Tumekuwa tukioa elimu na kupita kukagua nguruwe katika maeneo mabalimbali ya wilaya hii na tumefanikiwa kutokomeza ugonjwa huu japo haikuwa rahisi kwakuwa kuna baadhi ya watu wasio waaminifu walikuwa wakichinja kwa siri na kuuza nyama hiyo huku wakiwa wameipa jina la Mbolea ya Ruzuku ili wasigundulike kwa urahisi".

Chanzo:Wasafi media


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo