CCM kusimamia mchakato wa Katiba Mpya

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo, amesema kuwa shughuli ya usimamizi na uratibu wa upatikanaji wa Katiba Mpya ya kisasa utasimamiwa na chama hicho na si vinginevyo.


Chongolo ameitoa kauli hiyo hii jana Juni Mosi, 2023, mkoani Iringa wakati akihitimisha ziara yake mkoani humo iliyokuwa na lengo la kukagua utekelezwaji wa ilani ya chama hicho, kuangalia uimara wa chama pamoja na mambo mengine.

"Watu wanapigapiga kelele huko ngoja niwaambie, CCM ndiyo chama kiongozi, na ndiyo chama kitakachoongoza mchakato wa Katiba ya kisasa, iliyoandaliwa kisasa,na itatengenezwa kupitia mikono, uongozi, usimamizi na uratibu wa CCM na si vinginevyo," amesema Chongolo

Aidha Chongolo ameongeza kuwa, "Msidanganyike watu wengi wanataka Katiba kwa maslahi binafsi, wengi ukiangalia hawazungumzii pembejeo za kilimo, usalama wa Watanzania wala miundombinu ya barabara, wao wanataka tume hutu ya uchaguzi, wanataka mambo ambayo yatawapa nafasi ya kwenda kwenye madaraka."


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo