Chifu wa Kinyakyusa Akabidhiwa Ikulu Yake

Katika kutekeleza adhima ya Mhe Rais Samia Suluh Hassan ambaye ni kiongozi wa machifu nchini Chifu 'Hangaya' ya kuendeleza tamaduni za kichifu nchini, hatimaye Chifu wa kabila la Wanyakyusa, Chifu Edwin Mwakatumbula amekabidhiwa Ikulu yake ya Kichifu na kiongozi wa machifu wadogo wa kabila hilo.


Ikulu hiyo ipo katika Kijiji cha Masoko Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya.

Akizungumza katika tukio hilo la kihistoria, Chief Edwin amesema kuwa imekuwa siku ya baraka kwenye himaya hiyo, kwa yeye kukabidhiwa Ikulu hiyo iliyojengwa Mwaka 1,900 huku akiahidi kuendeleza umoja, mila na tamaduni za kabila hilo.

Amesema kuwa aliporithi uchifu wa kabila hilo kutoka kwa marehemu Chifu Daudi B Mwakatumbula miaka 10 iliyopita amejitahidi kuendeleza mila za kabila hizo huku akidumisha amani, umoja na mshikamano miongoni mwa Wanyakyusa wote nchini.

#edwinmoshiupdates


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo