Watu takribani 27 wamefariki dunia huku maelfu ya watu wakikosa makazi baada ya bwawa kubwa lililoko mjini Nakuru nchini Kenya kuvunja kuta zake siku ya Jumatano usiku.
Juhudi za ukoaji zinaendelea kufanywa na maafisa wa msalaba mwekundu wakisaidiana na vijana wa huduma za kitaifa.


