Kamanda wa Polisi mkoani Mtwara Lucas Mkondya amethibitisha kutokea kwa tukio hilo, na kusema kwamba mwanaume huyo anatuhumiwa kulawiti watoto watatu wenye miaka 13, 14 na 15, wa shule ya msingi Kawawa, walipokuwa wanatafuta Nazi kwenye minazi iliyopo vichakani baada ya kutoka shule.
Vitendo vya ukatili dhidi ya watoto vinazidi kushamiri nchini, ambapo hutishiwa na kufanyiwa ukatili huo.
Akizungumzia tukio hilo, kamanda wa polisi mkoa wa Mtwara, Lucas Mkondya, amesema watoto waliolawitiwa ni wenye umri chini ya miaka 15 ambapo mtuhumiwa huyo alienda nao porini na kuwatisha kwa panga kabla ya kuwafanyia tukio hilo.
